Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
Mara sita Amesema:
ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ
“… kisha akalingana juu ya ´Arshi.”[1]
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[2]
MAELEZO
Maeneo sita ndani ya Qur-aan imekuja:
ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ
“… kisha akalingana juu ya ´Arshi.”
Bi maana amepanda na kuwa juu yake. Kulingana ni moja miongoni mwa sifa za Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) za kimatendo, ilihali ujuu ni sifa ya kidhati. Tofauti kati ya ujuu wa Allaah na kulingana Kwake juu ni kwamba Allaah daima anasifika kuwa juu ilihali kulingana ni sifa ya kimatendo anayoifanya pale anapotaka. Ndio maana akasema:
ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ
“… kisha akalingana juu ya ´Arshi.”
Kielezi ”kisha” kinaonyesha mpangilio wa matukio. Kwa hivyo kulingana ni sifa ya kimatendo Anayoifanya wakati anapotaka (Subhaanahu wa Ta´ala), ilihali ujuu Wake ni sifa ya kidhati ambayo daima anasifika nayo. Katika Suurah ”al-A´raaf”, ”Yuunus”, ”ar-Ra´d”, ”Twaa Haa”, ”al-Furqaan”, ”as-Sajdah” na ”al-Hadiyd” Allaah amethibitisha kulingana juu ya ´Arshi.
[1] 07:54
[2] 20:05
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaaa al-Hamawiyyah, uk. 112-113
- Imechapishwa: 20/08/2024
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
Mara sita Amesema:
ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ
“… kisha akalingana juu ya ´Arshi.”[1]
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
”Mwingi wa rehema amelingana juu ya ´Arshi.”[2]
MAELEZO
Maeneo sita ndani ya Qur-aan imekuja:
ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ
“… kisha akalingana juu ya ´Arshi.”
Bi maana amepanda na kuwa juu yake. Kulingana ni moja miongoni mwa sifa za Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) za kimatendo, ilihali ujuu ni sifa ya kidhati. Tofauti kati ya ujuu wa Allaah na kulingana Kwake juu ni kwamba Allaah daima anasifika kuwa juu ilihali kulingana ni sifa ya kimatendo anayoifanya pale anapotaka. Ndio maana akasema:
ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ
“… kisha akalingana juu ya ´Arshi.”
Kielezi ”kisha” kinaonyesha mpangilio wa matukio. Kwa hivyo kulingana ni sifa ya kimatendo Anayoifanya wakati anapotaka (Subhaanahu wa Ta´ala), ilihali ujuu Wake ni sifa ya kidhati ambayo daima anasifika nayo. Katika Suurah ”al-A´raaf”, ”Yuunus”, ”ar-Ra´d”, ”Twaa Haa”, ”al-Furqaan”, ”as-Sajdah” na ”al-Hadiyd” Allaah amethibitisha kulingana juu ya ´Arshi.
[1] 07:54
[2] 20:05
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat at-Tawdhwiyhiyyah ´alaa Muqaddimat-il-Fatwaaa al-Hamawiyyah, uk. 112-113
Imechapishwa: 20/08/2024
https://firqatunnajia.com/75-tofauti-kati-ya-kuwa-juu-kwa-allaah-na-kulingana-kwake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)