73 – Mu´aadh bin Jabal amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Wale wanaopendana kwa ajili ya Allaah atawaweka chini ya kivuli cha ´Arshi Yake Siku ambayo hakuna kivuli kingine isipokuwa kivuli Chake.”[1]

[1] Swahiyh. Ameipokea Ahmad (5/229, 236 na 237), Ibn Hibbaan (2510), al-Haakim (4/169-170) na Ibn-ul-Mubaarak katika “az-Zuhd” (715) kupitia njia mbili zingine Swahiyh. Moja katika njia hizo mbili ameisahihisha al-Haakim kwa mujibu wa sharti za al-Bukhaariy na Muslim na adh-Dhahabiy akaafikiana naye. Hata hivyo usahihishaji huo unatakiwa kuangaliwa vyema, kama nilivyobainisha katika “Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb” (4/47).

  • Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk. 112-113
  • Imechapishwa: 26/06/2024
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy