Baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumaliza Rak´ah ya pili alikuwa akikaa katika Tashahhud. Swalah ikiwa ya Rak´ah mbili, kama vile Fajr, basi hukaa kama vile anavyokaa kati ya Sujuud mbili[1]. Hivyo ndivyo alivyokuwa akikaa kwenye Tashahhud ya kwanza katika zile swalah zilizo na Rak´ah tatu na Rak´ah nne[2].
Vivyo hivyo alimuamrisha yule mtu aliyeswali kimakosa na kumwambia:
“Unapokaa katikati ya swalah basi tulizana, tandaza paja lako la kushoto kisha usome Tashahhud.”[3]
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Kipenzi changu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alinikataza kuchutama kama achutamavyo mbwa.”[4]
Katika Hadiyth nyingine imekuja:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akikataza kizingiti cha shaytwaan.”[5]
Alipokuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akikaa katika Tashahhud alikuwa akiweka kitanga chake cha mkono wa kulia juu ya paja lake la kulia[6] na kitanga cha mkono wake wa kushoto[7] juu ya paja lake la kushoto[8].
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiweka kisugudi chake cha mkono wa kulia[9] juu ya paji lake la kulia[10].
Alimkataza (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mwanaume mmoja ambaye alikuwa ameketi katika swalah hali ya kuegemea mkono wake wa kushoto na akamwambia:
“Hiyo ni swalah ya mayahudi.”[11]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Usiketi namna hiyo. Hivyo huketi wale wanaoadhibiwa.”[12]
Katika Hadiyth nyingine imekuja:
“Hivyo ndivyo huketi wale walioghadhibikiwa.”[13]
[1] an-Nasaa’iy (1/173) kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh.
[2] al-Bukhaariy na Abu Daawuud.
[3] Abu Daawuud na al-Bayhaqiy kwa mlolongo wa wapokezi mzuri.
[4] at-Twayaalisiy, Ahmad na Ibn Abiy Shaybah. Abu ´Ubaydah na wengineo wamesema kuhusu kuhusu al-Iq´aa´:
“Ni pale mtu anapogandamiza kikalio chake kwenye ardhi, anaweka muundi wake wima na mikono mbele yake kama afanyavyo mbwa.”
Hii sio ile al-Iq´aa´ inayokubalika katika Shari´ah baina ya Sujuud mbili, kama ilivyotangulia.
[5] Muslim, Abu ´Awaanah na wengineo. Imetajwa katika ”al-Irwaa’” (316).
[6] Katika upokezi mwingine imekuja “kwenye goti lake la kulia”.
[7] Katika upokezi mwingine imekuja “kwenye goti lake la kushoto”.
[8] Muslim na Abu ´Awaanah.
[9] Inavyoonekana ni kwamba hakutenganisha viwiko vyake na mbavu zake, kama alivyoweka wazi hilo Ibn-ul-Qayyim katika “Zaad-ul-Ma´aad”.
[10] Abu Daawuud na an-Nasaa’iy kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh.
[11] al-Bayhaqiy na al-Haakim aliyeisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye. Hiyo na Hadiyth ya kufuata zimetajwa katika “al-Irwaa´” (380).
[12] Ahmad na Abu Daawuud kwa mlolongo wa wapokezi mzuri.
[13] ´Abdur-Razzaaq. Swahiyh kwa mujibu wa ´Abdul-Haqq katika ”al-Ahkaam” (1284 kwa uhakiki wangu).
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 136-137
- Imechapishwa: 20/08/2017
Baada ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumaliza Rak´ah ya pili alikuwa akikaa katika Tashahhud. Swalah ikiwa ya Rak´ah mbili, kama vile Fajr, basi hukaa kama vile anavyokaa kati ya Sujuud mbili[1]. Hivyo ndivyo alivyokuwa akikaa kwenye Tashahhud ya kwanza katika zile swalah zilizo na Rak´ah tatu na Rak´ah nne[2].
Vivyo hivyo alimuamrisha yule mtu aliyeswali kimakosa na kumwambia:
“Unapokaa katikati ya swalah basi tulizana, tandaza paja lako la kushoto kisha usome Tashahhud.”[3]
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Kipenzi changu (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alinikataza kuchutama kama achutamavyo mbwa.”[4]
Katika Hadiyth nyingine imekuja:
“Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akikataza kizingiti cha shaytwaan.”[5]
Alipokuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akikaa katika Tashahhud alikuwa akiweka kitanga chake cha mkono wa kulia juu ya paja lake la kulia[6] na kitanga cha mkono wake wa kushoto[7] juu ya paja lake la kushoto[8].
Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akiweka kisugudi chake cha mkono wa kulia[9] juu ya paji lake la kulia[10].
Alimkataza (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) mwanaume mmoja ambaye alikuwa ameketi katika swalah hali ya kuegemea mkono wake wa kushoto na akamwambia:
“Hiyo ni swalah ya mayahudi.”[11]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Usiketi namna hiyo. Hivyo huketi wale wanaoadhibiwa.”[12]
Katika Hadiyth nyingine imekuja:
“Hivyo ndivyo huketi wale walioghadhibikiwa.”[13]
[1] an-Nasaa’iy (1/173) kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh.
[2] al-Bukhaariy na Abu Daawuud.
[3] Abu Daawuud na al-Bayhaqiy kwa mlolongo wa wapokezi mzuri.
[4] at-Twayaalisiy, Ahmad na Ibn Abiy Shaybah. Abu ´Ubaydah na wengineo wamesema kuhusu kuhusu al-Iq´aa´:
“Ni pale mtu anapogandamiza kikalio chake kwenye ardhi, anaweka muundi wake wima na mikono mbele yake kama afanyavyo mbwa.”
Hii sio ile al-Iq´aa´ inayokubalika katika Shari´ah baina ya Sujuud mbili, kama ilivyotangulia.
[5] Muslim, Abu ´Awaanah na wengineo. Imetajwa katika ”al-Irwaa’” (316).
[6] Katika upokezi mwingine imekuja “kwenye goti lake la kulia”.
[7] Katika upokezi mwingine imekuja “kwenye goti lake la kushoto”.
[8] Muslim na Abu ´Awaanah.
[9] Inavyoonekana ni kwamba hakutenganisha viwiko vyake na mbavu zake, kama alivyoweka wazi hilo Ibn-ul-Qayyim katika “Zaad-ul-Ma´aad”.
[10] Abu Daawuud na an-Nasaa’iy kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh.
[11] al-Bayhaqiy na al-Haakim aliyeisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye. Hiyo na Hadiyth ya kufuata zimetajwa katika “al-Irwaa´” (380).
[12] Ahmad na Abu Daawuud kwa mlolongo wa wapokezi mzuri.
[13] ´Abdur-Razzaaq. Swahiyh kwa mujibu wa ´Abdul-Haqq katika ”al-Ahkaam” (1284 kwa uhakiki wangu).
Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 136-137
Imechapishwa: 20/08/2017
https://firqatunnajia.com/69-tashahhud-ya-kwanza-na-vikao-vyake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)