al-Qummiy amesema pindi alipokuwa akifasiri Aayah:
وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّـهِ جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا
“Na shikamaneni kwa kamba ya Allaah nyote pamoja na wala msifarikiane!”[1]
“Upwekeshaji na uongozi. Abul-Jaaruud amepokea kupitia kwa Abu Ja´far aliyesema: “Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) alijua kuwa watatofautiana baada ya Mtume wao. Ndio maana Akawakataza kufarikiana na akawaamrisha kukusanyika juu ya uongozi wa familia ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[2]
Kushikamana na kamba ya Allaah ni Qur-aan na Sunnah na I´tiqaad, hukumu, mu´amala na Shari´ah zengine zilizomo ndani yake. Mazanadiki hawa wanawakimbiza watu kutoka katika ´Aqiydah na matendo haya na kuwavuta katika ´Aqiydah ya Raafidhwah ambayo inaipiga vita Qur-aan, Sunnah, waislamu na khaswa ´Aliy na familia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
´Aliy na familia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wameamrishwa kushikamana na Qur-aan na Sunnah na wamekatazwa kufarikiana. Kile chenye kufanya kazi kwa waislamu kinawagusa wao pia. Wao ni watu wa kawaida ambao wanapatia na kukosea. Yale wanayoyasema ambayo yanaafikiana na Qur-aan na Sunnah, ni wajibu kuyakubali, na yale wanayokosea haijuzu kuyakubali. Yale yenye kufanya kazi kwa wanachuoni wa waislamu katika Maswahabah, Taabi´uun, waliokuja baada ya Taabi´uun na waliokuja baada yao, kinafanya kazi vilevile kwao pia; maneno ya kila mmoja yanakubaliwa na kukataliwa.
[1] 03:103
[2] Tafsiyr al-Qummiy (1/108).
- Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 103
- Imechapishwa: 03/04/2017
al-Qummiy amesema pindi alipokuwa akifasiri Aayah:
وَاعْتَصِمُوا بِحَبْلِ اللَّـهِ جَمِيعًا وَلَا تَفَرَّقُوا
“Na shikamaneni kwa kamba ya Allaah nyote pamoja na wala msifarikiane!”[1]
“Upwekeshaji na uongozi. Abul-Jaaruud amepokea kupitia kwa Abu Ja´far aliyesema: “Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) alijua kuwa watatofautiana baada ya Mtume wao. Ndio maana Akawakataza kufarikiana na akawaamrisha kukusanyika juu ya uongozi wa familia ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[2]
Kushikamana na kamba ya Allaah ni Qur-aan na Sunnah na I´tiqaad, hukumu, mu´amala na Shari´ah zengine zilizomo ndani yake. Mazanadiki hawa wanawakimbiza watu kutoka katika ´Aqiydah na matendo haya na kuwavuta katika ´Aqiydah ya Raafidhwah ambayo inaipiga vita Qur-aan, Sunnah, waislamu na khaswa ´Aliy na familia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
´Aliy na familia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wameamrishwa kushikamana na Qur-aan na Sunnah na wamekatazwa kufarikiana. Kile chenye kufanya kazi kwa waislamu kinawagusa wao pia. Wao ni watu wa kawaida ambao wanapatia na kukosea. Yale wanayoyasema ambayo yanaafikiana na Qur-aan na Sunnah, ni wajibu kuyakubali, na yale wanayokosea haijuzu kuyakubali. Yale yenye kufanya kazi kwa wanachuoni wa waislamu katika Maswahabah, Taabi´uun, waliokuja baada ya Taabi´uun na waliokuja baada yao, kinafanya kazi vilevile kwao pia; maneno ya kila mmoja yanakubaliwa na kukataliwa.
[1] 03:103
[2] Tafsiyr al-Qummiy (1/108).
Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 103
Imechapishwa: 03/04/2017
https://firqatunnajia.com/65-al-qummiy-upotoshaji-wake-wa-tano-wa-aal-imraan/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)