152 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Anapochemua mmoja wenu, basi aseme:
الْحَمْـدُ للهِ
“Himdi zote ni stahiki ya Allaah.”
Ndugu au rafiki yake amwambie:
يَرْحَمُـكَ الله
“Allaah akurehemu.”
Atakapoambiwa hivo basi aseme tena:
يَهْـديكُـمُ اللهُ وَيُصْـلِحُ بالَـكُم
“Allaah awaongoze na ayatengeneze mambo yenu.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy.
MAELEZO
Katika Hadiyth kuna faida zifuatazo:
1 – Uwekwaji Shari´ah wa kumhimidi Allaah baada ya kuchemua kwa yeye kusema:
الحمد لله رب العالمين
“Himdi zote njema anastahiki Allaah, Mola wa walimwengu.”
au:
الحمد لله
“Himdi zote njema anastahiki Allaah.”
2 – Uwekwaji Shari´ah wa kumtakia rehema mchemuaji akimuhimidi Allaah kwa njia ya kwamba msemaji amwambie:
يَرْحَمُـكَ الله
“Allaah akurehemu.”
Asipomshukuru Allaah basi hatotakiwa rehema. Imepokelewa katika Hadiyth ya kwamba kuna watu wawili waliochemua mbele ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akamtakia rehema yule mmoja na hakumtakia rehema yule mwingine. Akasema yule bwana ambaye hakumtakia rehema: “Amechemua fulani ukamtakia rehema na mimi nimechemua hukunitakia rehema. Ndipo akasema:
“Huyu amemuhimidi Allaah na wewe hukumuhimidi Allaah.”[2]
[1] al-Bukhaariy (6224).
[2] Muslim (2991).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 144
- Imechapishwa: 16/11/2025
152 – Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Anapochemua mmoja wenu, basi aseme:
الْحَمْـدُ للهِ
“Himdi zote ni stahiki ya Allaah.”
Ndugu au rafiki yake amwambie:
يَرْحَمُـكَ الله
“Allaah akurehemu.”
Atakapoambiwa hivo basi aseme tena:
يَهْـديكُـمُ اللهُ وَيُصْـلِحُ بالَـكُم
“Allaah awaongoze na ayatengeneze mambo yenu.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy.
MAELEZO
Katika Hadiyth kuna faida zifuatazo:
1 – Uwekwaji Shari´ah wa kumhimidi Allaah baada ya kuchemua kwa yeye kusema:
الحمد لله رب العالمين
“Himdi zote njema anastahiki Allaah, Mola wa walimwengu.”
au:
الحمد لله
“Himdi zote njema anastahiki Allaah.”
2 – Uwekwaji Shari´ah wa kumtakia rehema mchemuaji akimuhimidi Allaah kwa njia ya kwamba msemaji amwambie:
يَرْحَمُـكَ الله
“Allaah akurehemu.”
Asipomshukuru Allaah basi hatotakiwa rehema. Imepokelewa katika Hadiyth ya kwamba kuna watu wawili waliochemua mbele ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo akamtakia rehema yule mmoja na hakumtakia rehema yule mwingine. Akasema yule bwana ambaye hakumtakia rehema: “Amechemua fulani ukamtakia rehema na mimi nimechemua hukunitakia rehema. Ndipo akasema:
“Huyu amemuhimidi Allaah na wewe hukumuhimidi Allaah.”[2]
[1] al-Bukhaariy (6224).
[2] Muslim (2991).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 144
Imechapishwa: 16/11/2025
https://firqatunnajia.com/64-duaa-wakati-wa-kuchemua-2/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
