58 – Ibn Mas´uud amesema kuhusu Aayah:

بَلْ أَحْيَاءٌ عِندَ رَبِّهِمْ يُرْزَقُونَ

”Bali wahai kwa Mola wao wanaruzukiwa.”[1]

”Tuliuliza juu ya hilo. Wakasema: ”Roho zao zimo ndani ya matumbo ya kijani ya ndege. Zinaruka Peponi popote zinapotaka. Kisha zinarudi kwenye taa zilizoning´inia kwenye taa za ´Arshi. Wakati watapokuwa katika hali hiyo, tahamaki Atawadhihirikia Mola wako na kusema: ”Niombeni mtakacho!”

Ameipokea Muslim, at-Tirmidhiy na al-Qazwiyniy.

[1] 3:169

  • Mhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Ahmad adh-Dhahabiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Mukhtasar-ul-´Uluww, uk. 105-106
  • Imechapishwa: 26/06/2024
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy