Swali 61: Hadiyth ya ´Umm ´Atwiyyah:
“Tumekatazwa kufuata jeneza na wala hatukutiliwa mkazo.”[1]
Ifahamike vipi?
Jibu: Inafahamika kwamba kwa mtazamo wake makatazo hayakutiliwa mkazo. Kimsingi ni kwamba makatazo yanapelekea katika uharamu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yale niliyokukatazeni basi jiepusheni nayo na yale niliyokuamrisheni basi yaendeeni kiasi muwezavyo.”[2]
Kuna maafikiano juu ya usahihi wake.
Hiyo inajulisha juu ya uharamu wa wanawake kuyasindikiza majeneza kwenda makaburini. Kuhusu kumswalia maiti ni jambo limewekwa katika Shari´ah kwao kama wanamme.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/178).
[2] Ahmad (7288) na Muslim (1337).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 45-46
- Imechapishwa: 26/12/2021
Swali 61: Hadiyth ya ´Umm ´Atwiyyah:
“Tumekatazwa kufuata jeneza na wala hatukutiliwa mkazo.”[1]
Ifahamike vipi?
Jibu: Inafahamika kwamba kwa mtazamo wake makatazo hayakutiliwa mkazo. Kimsingi ni kwamba makatazo yanapelekea katika uharamu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yale niliyokukatazeni basi jiepusheni nayo na yale niliyokuamrisheni basi yaendeeni kiasi muwezavyo.”[2]
Kuna maafikiano juu ya usahihi wake.
Hiyo inajulisha juu ya uharamu wa wanawake kuyasindikiza majeneza kwenda makaburini. Kuhusu kumswalia maiti ni jambo limewekwa katika Shari´ah kwao kama wanamme.
[1] Majmuu´-ul-Fataawaa (13/178).
[2] Ahmad (7288) na Muslim (1337).
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz, uk. 45-46
Imechapishwa: 26/12/2021
https://firqatunnajia.com/61-mwanamke-amekatazwa-kusindikiza-jeneza-makaburini-ii/