148 – ´Abdullaah bin Abiy Awfaa (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliomba siku ya Ahzaab dhidi ya washirikina akasema:
اللَّهُمَّ مُنْزِلَ الكِتَابِ، سَرِيعَ الحِسَابِ، اللَّهُمَّ اهْزِمِ الأَحْزَابَ اللَّهُمَّ اهْزِمْهُمْ وَزَلْزِلْهُمْ
”Ee Allaah! Mteremsha wa Kitabu, mfanya haraka kuhesabu. Ee Allaah! Vishinde vikosi. Ee Allaah! Washinde na watetemeshe.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hii ndani yake kuna kuomba du´aa dhidi ya washirikina wakati wamekusanyika vikundi, kukandamiza na kudhuru. Kwa hiyo ni lazima kwa kila muislamu kumuomba Allaah (´Azza wa Jall) kwa mfano wa du´aa hii awatetemeshe washirikina na makundi yale ambayo yalikusanyika dhidi ya waislamu. Aidha aingize khofu ndani ya nyoyo zao, asambaratishe umoja wao, awaparanganishe na akate mizizi yao na atutosheleze sisi na waislamu wengine kutokana na shari yao.
[1] al-Bukhaariy (2933) na Muslim (1742).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 140
- Imechapishwa: 15/11/2025
148 – ´Abdullaah bin Abiy Awfaa (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliomba siku ya Ahzaab dhidi ya washirikina akasema:
اللَّهُمَّ مُنْزِلَ الكِتَابِ، سَرِيعَ الحِسَابِ، اللَّهُمَّ اهْزِمِ الأَحْزَابَ اللَّهُمَّ اهْزِمْهُمْ وَزَلْزِلْهُمْ
”Ee Allaah! Mteremsha wa Kitabu, mfanya haraka kuhesabu. Ee Allaah! Vishinde vikosi. Ee Allaah! Washinde na watetemeshe.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hii ndani yake kuna kuomba du´aa dhidi ya washirikina wakati wamekusanyika vikundi, kukandamiza na kudhuru. Kwa hiyo ni lazima kwa kila muislamu kumuomba Allaah (´Azza wa Jall) kwa mfano wa du´aa hii awatetemeshe washirikina na makundi yale ambayo yalikusanyika dhidi ya waislamu. Aidha aingize khofu ndani ya nyoyo zao, asambaratishe umoja wao, awaparanganishe na akate mizizi yao na atutosheleze sisi na waislamu wengine kutokana na shari yao.
[1] al-Bukhaariy (2933) na Muslim (1742).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 140
Imechapishwa: 15/11/2025
https://firqatunnajia.com/61-duaa-dhidi-ya-adui/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
