Swali: Allaah (Ta´ala) amesema:
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
“Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa.”[1]
Je, hili ni jambo linalowahusu waislamu peke yao pasi na makafiri hata kama makafiri hao watakuwa wasafi?
Jibu: Imesemekana kwamba:
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
“Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa.”[2]
wanaokusudiwa ni Malaika. Kuna maoni vilevile yanayosema kwamba inawahusu vilevile wanaadamu. Wako ambao wanaona kuwa Qur-aan haiguswi isipokuwa na ambaye ametawadha. Dalili juu ya hilo ni ile barua ambayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwandikia ´Amr bin Hamz:
“Asiiguse Qur-aan isipokuwa aliye msafi.”
Japokuwa tafsiri ya Aayah hapo juu inahusu Ubao uliohifadhiwa na wagusaji hapo ni Malaika lakini kadhalika Qur-aan haitakiwi kuguswa isipokuwa na ambaye ametawadha.
Kuhusu kafiri hatakiwi kuigusa Qur-aan wala hatakiwi kuachwa akaigusa.
[1] 56:79
[2] 56:79
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (05) http://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191110#219240
- Imechapishwa: 21/09/2019
Swali: Allaah (Ta´ala) amesema:
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
“Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa.”[1]
Je, hili ni jambo linalowahusu waislamu peke yao pasi na makafiri hata kama makafiri hao watakuwa wasafi?
Jibu: Imesemekana kwamba:
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
“Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa.”[2]
wanaokusudiwa ni Malaika. Kuna maoni vilevile yanayosema kwamba inawahusu vilevile wanaadamu. Wako ambao wanaona kuwa Qur-aan haiguswi isipokuwa na ambaye ametawadha. Dalili juu ya hilo ni ile barua ambayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwandikia ´Amr bin Hamz:
“Asiiguse Qur-aan isipokuwa aliye msafi.”
Japokuwa tafsiri ya Aayah hapo juu inahusu Ubao uliohifadhiwa na wagusaji hapo ni Malaika lakini kadhalika Qur-aan haitakiwi kuguswa isipokuwa na ambaye ametawadha.
Kuhusu kafiri hatakiwi kuigusa Qur-aan wala hatakiwi kuachwa akaigusa.
[1] 56:79
[2] 56:79
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (05) http://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191110#219240
Imechapishwa: 21/09/2019
https://firqatunnajia.com/59285-2/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)