Abu Ja´far at-Twahaawiy (Rahimahu Allaah) amesema:
88 – Tunawapenda watu waadilifu na waaminifu, na tunawachukia watu wa dhuluma na khiyana.
89 – Katika yale ambayo hatuna uhakika nayo tunasema “Allaah ndiye mjuzi zaidi”.
90 – Tunaona kufaa kufuta juu ya soki za ngozi, ni mamoja wakati wa safari na mjini. Hivyo ndivyo imepokelewa.
MAELEZO
Kama waandishi wengine walioandika juu ya vitabu vya ´Aqiydah, mtunzi ameingiza suala la kufuta juu ya soksi za ngozi pasi na kutaja kufuta juu ya soksi za kawaida na viatu. Hilo ni kutokana na sababu mbili:
1 – Kupangusa juu ya soksi za ngozi ni jambo limepokelewa kwa mapokezi mengi kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
2 – Raafidhwah wanapinga Sunnah hii. Kwa ajili hiyo hoja ni yenye nguvu zaidi dhidi yao kwa yale yaliyopokelewa kwa mapokezi mengi kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Kwa sababu tu kumetajwa soksi za ngozi, haina maana kuwa kupangusa soksi za kawaida na viatu havikuthibiti. Unaweza kusoma kwa undani zaidi jambo hilo katika ”al-Mas´h ´alaal-Jawrabayn” cha Shaykh al-Qaasimiy, ambacho nimekiambatanishia kiambatisho na hukumu kadhaa zinazohusiana na kupangusa.
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah – Sharh wa Ta´liyq, uk. 81-82
- Imechapishwa: 09/10/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)