Imaam Ibn Abiy Daawuud (Rahimahu Allaah) amesema:
وسبطي رسول الله وابني خديجة
21 – Vilevile wajukuze Mtume wa Allaah na wana wa Khadiyjah
وفاطمة ذات النقاء تبحبحوا
na Faatwimah mwenye kusifiwa
وعائشـة أم المؤمنين وخالنـا
22 – Vilevile na ´Aaishah ambaye ni mama wa waumini, na mjomba wetu
معـاوية أكـرم به ثم امـنح
ambaye si mwengine ni Mu´aawiyah muheshimiwa
MAELEZO
Maneno yake mtunzi (Rahimahu Allaah):
“Wajukuze Mtume wa Allaah.”
Bi maana al-Hasan na al-Husayn (Radhiya Allaahu ´anhumaa). al-Hasan na al-Husayn ni wajukuze wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Bi maana ni watoto wa msichana wake Faatwimah. Wao ndio:
“Viongozi wa vijana wa Peponi.”[1]
kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“… wana wa Khadiyjah.”
Watoto wote wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wanatokamana na Khadiyjah. Isipokuwa Ibraahiym peke yake. Yeye mama yake ni Maariyah Qibtwiyyah. Kuhusu watoto wengine wote wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wanatokamana na Khadiyjah (Radhiya Allaahu ´anhaa). Alizaa nae wavulana wawili waliokufa katika uhai wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika mji wa Makkah.
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“… na Faatwimah.”
Faatwimah ambaye ni binti yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa anampenda. Faatwimah alipokuwa anafika anasimama kwa ajili yake na kumbusu na kumkalisha pembezoni nae.
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“Vilevile na ´Aaishah ambaye ni mama wa waumini… “
Yeye ndiye mwanamke aliyekuwa akipendwa zaidi na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Mwanaume aliyekuwa akipendwa zaidi na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni baba yake ambaye ni Abu Bakr asw-Swiddiyq (Radhiya Allaahu ´anh)[2].
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amesema:
“… mjomba wetu ambaye si mwengine ni Mu´aawiyah.”
Mu´aawiyah bin Abiy Sufyaan (Radhiya Allaahu ´anh). Huyu alikuwa ni Swahabah mtukufu. Alikuwa ni mwandishi wa Wahy. Alikuwa akimwandikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Qur-aan. Alikuwa ni mjomba wa waumini kwa sababu dada yake, ambaye ni Umm Habiybah, ni mkewe Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hivyo yeye anakuwa ni mjomba wa waumini. Bi maana yeye ni kaka wa mama wa waumini. Hizi ni katika fadhilah zake (Radhiya Allaahu ´anh).
[1] Kuna idadi kubwa ya Maswahabah (Radhiya Allaahu ´anhum) ambao wamepokea Hadiyth hii mpaka as-Suyuutwiy akasema: “Hili ni jambo limepokelewa kwa njia nyingi.” Faydhw-ul-Qadiyr (03/415)
[2] Ameyapokea haya al-Bukhaariy (4358) na (3662) na Muslim (08) na (2384)
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh al-Mandhuumat-ul-Haaiyyah fiy ´Aqiydati Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 127-128
- Imechapishwa: 10/01/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)