53. Kila mtu anaweza kupata ulimwengu na si dini

209 – Abu Bakr ametukhabarisha: Ibn Numayr ametukhabarisha: Abaan bin Ishaaq ametukhabarisha, kutoka kwa as-Swabbaah bin Muhammad, kutoka kwa Murrah al-Hamadaaniy, kutoka kwa ´Abdullaah bin Mas´uud, ambaye amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amezigawanya baina yenu tabia zenu kama vile amegawanya baina yenu riziki zenu. Allaah humpa dunia anayempenda na asiyempenda, lakini hampi dini isipokuwa anayempenda. Hivyo basi, anyempa dini basi amempenda.”[1]

[1] Ahmad (3663). Dhaifu kwa mujibu wa Ahmad Shaakir na dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Dhwa´iyf-ul-Jaamiy´” (1894).

  • Muhusika: Imaam Abu Bakr Ahmad bin Abiy ´Aaswim ash-Shaybaaniy (a.f.k. 287)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Kitaab-uz-Zuhd, uk. 54
  • Imechapishwa: 16/07/2025