137 – ´Uthmaan bin Abiyl-´Aasw ath-Thaqafiy amesimulia: “Nilimshtakia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) maumivu ninayohisi mwilini mwangu tangu niliposilimu.” Ndipo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwambia: “Weka mkono wako pale mahali unapohisi maumivu katika mwili wako, useme mara tatu:
باسم الله
“Kwa jina la Allaah.”
kisha useme mara saba:
أَعُوذُ بِاللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأُحَاذِرُ
“Najilinda kwa Allaah na kwa uwezo Wake kutokamana na shari ya ninachokihisi na ninachokitahadhari.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Katika Hadiyth hii kuna uwekwaji Shari´ah wa mtu kuweka mkono wake pale mahali anapohisi maumivu mwilini mwake na aseme Dhikr hii mara tatu:
باسم الله
“Kwa jina la Allaah.”
kisha useme mara saba:
أَعُوذُ بِاللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأُحَاذِرُ
“Najilinda kwa Allaah na kwa uwezo Wake kutokamana na shari ya ninachokihisi na ninachokitahadhari nacho.”
Imekuja katika tamko jengine:
أَعُوذُ بِعِزَّةِ اللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأَحَاذِرُ
“Najilinda kwa utukufu wa Allaah na kwa uwezo Wake kutokamana na shari ya ninachokihisi na ninachokitahadhari nacho.”[2]
[1] Muslim (2203).
[2] Abu Daawuud (3891), at-Tirmidhiy (2080) na Ibn Maajah (3522).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 132
- Imechapishwa: 12/11/2025
137 – ´Uthmaan bin Abiyl-´Aasw ath-Thaqafiy amesimulia: “Nilimshtakia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) maumivu ninayohisi mwilini mwangu tangu niliposilimu.” Ndipo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwambia: “Weka mkono wako pale mahali unapohisi maumivu katika mwili wako, useme mara tatu:
باسم الله
“Kwa jina la Allaah.”
kisha useme mara saba:
أَعُوذُ بِاللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأُحَاذِرُ
“Najilinda kwa Allaah na kwa uwezo Wake kutokamana na shari ya ninachokihisi na ninachokitahadhari.”[1]
Ameipokea Muslim.
MAELEZO
Katika Hadiyth hii kuna uwekwaji Shari´ah wa mtu kuweka mkono wake pale mahali anapohisi maumivu mwilini mwake na aseme Dhikr hii mara tatu:
باسم الله
“Kwa jina la Allaah.”
kisha useme mara saba:
أَعُوذُ بِاللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأُحَاذِرُ
“Najilinda kwa Allaah na kwa uwezo Wake kutokamana na shari ya ninachokihisi na ninachokitahadhari nacho.”
Imekuja katika tamko jengine:
أَعُوذُ بِعِزَّةِ اللَّهِ وَقُدْرَتِهِ مِنْ شَرِّ مَا أَجِدُ وَأَحَاذِرُ
“Najilinda kwa utukufu wa Allaah na kwa uwezo Wake kutokamana na shari ya ninachokihisi na ninachokitahadhari nacho.”[2]
[1] Muslim (2203).
[2] Abu Daawuud (3891), at-Tirmidhiy (2080) na Ibn Maajah (3522).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 132
Imechapishwa: 12/11/2025
https://firqatunnajia.com/53-duaa-wakati-wa-kuhisi-maumivu-maeneo-fulani-mwilini/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
