133 – Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika Allaah anaridhia kwa mja kuwa anapokula mlo basi akamuhimidi kwacho au akanywa kinywaji basi akamuhimidi kwacho.”[1]
Ameipokea Muslim.
134 – Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia:“Alikuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pindi anapomaliza chakula chake husema:
الْحَمْـدُ للهِ حَمْـداً كَثـيراً طَيِّـباً مُبـارَكاً فيه، [غَيْرَ مَكْفِيٍّ] وَلا مُوَدَّعٍ وَلا مُسْتَغْـنىً عَنْـهُ رَبُّـنا
“Himdi zote njema anastahiki Allaah, himdi nyingi, nzuri, zenye baraka ndani yake [zisizorudishwa] wala kuagwa, wala kutoshwa nazo, Mola wetu.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
الحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي كَفَانَا وَأَرْوَانَا ، غَيْرَ مَكْفِي وَلَا مَكْفُورٍ ، وَقَالَ مَرَّةً : الحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّنَا ، غَيْرَ مَكْفِيٌّ وَلَا مُوَدَّعِ وَلَا مُسْتَغْنِّى ، رَبَّنَا
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye ametutosheleza na kutupa tunachohitaji, zisizorudishwa wala kukanushwa.”
Mara nyingine akisema:
“Himdi zote njema anastahiki Allaah, Mola wetu, zisizorudishwa wala kuagwa, wala kutoshwa nazo, Mola wetu.”[2]
Ameipokea al-Bukhaariy.
MAELEZO
Katika Hadiyth hii kuna mapendekezo ya kumhimidi Allaah (´Azza wa Jall) wakati wa kula na kunywa na baada ya kula na kunywa. Jengine ni kwamba kufanya hivo ni miongoni mwa sababu za kumridhisha Allaah (´Azza wa Jall).
[1] Muslim (2734).
[2] al-Bukhaariy (5458).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 129-130
- Imechapishwa: 11/11/2025
133 – Anas bin Maalik (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika Allaah anaridhia kwa mja kuwa anapokula mlo basi akamuhimidi kwacho au akanywa kinywaji basi akamuhimidi kwacho.”[1]
Ameipokea Muslim.
134 – Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia:“Alikuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pindi anapomaliza chakula chake husema:
الْحَمْـدُ للهِ حَمْـداً كَثـيراً طَيِّـباً مُبـارَكاً فيه، [غَيْرَ مَكْفِيٍّ] وَلا مُوَدَّعٍ وَلا مُسْتَغْـنىً عَنْـهُ رَبُّـنا
“Himdi zote njema anastahiki Allaah, himdi nyingi, nzuri, zenye baraka ndani yake [zisizorudishwa] wala kuagwa, wala kutoshwa nazo, Mola wetu.”
Imekuja katika upokezi mwingine:
الحَمْدُ لِلَّهِ الَّذِي كَفَانَا وَأَرْوَانَا ، غَيْرَ مَكْفِي وَلَا مَكْفُورٍ ، وَقَالَ مَرَّةً : الحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّنَا ، غَيْرَ مَكْفِيٌّ وَلَا مُوَدَّعِ وَلَا مُسْتَغْنِّى ، رَبَّنَا
“Himdi zote njema anastahiki Allaah ambaye ametutosheleza na kutupa tunachohitaji, zisizorudishwa wala kukanushwa.”
Mara nyingine akisema:
“Himdi zote njema anastahiki Allaah, Mola wetu, zisizorudishwa wala kuagwa, wala kutoshwa nazo, Mola wetu.”[2]
Ameipokea al-Bukhaariy.
MAELEZO
Katika Hadiyth hii kuna mapendekezo ya kumhimidi Allaah (´Azza wa Jall) wakati wa kula na kunywa na baada ya kula na kunywa. Jengine ni kwamba kufanya hivo ni miongoni mwa sababu za kumridhisha Allaah (´Azza wa Jall).
[1] Muslim (2734).
[2] al-Bukhaariy (5458).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 129-130
Imechapishwa: 11/11/2025
https://firqatunnajia.com/50-duaa-ya-kumshukuru-allaah-baada-ya-kula-na-kunywa/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
