Allaah (Ta´ala) amesema:
وَنَزَّلْنَا عَلَيْكَ الْكِتَابَ تِبْيَانًا لِّكُلِّ شَيْءٍ
“Na Tumekuteremshia Kitabu hali ya kuwa ni chenye kubainisha kila kitu.” (16:89)
an-Nasaa´iy na wengine wamepokea ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliona mikononi mwa ´Umar bin al-Khattwaab (Radhiya Allaahu ´anh) karatasi ya Tawraat akasema:
“Ee mwana wa al-Khattwaab! Una shaka? Nimekufikishieni waziwazi kabisa. Lau Muusa angelikuwa hai hii leo mkamfuata badala ya kunifuata mimi basi mgelikuwa mmepotea.” Ndipo ´Umar akasema: “Nimeridhia Allaah kuwa Mola Wangu, Uislamu kuwa dini yangu na Muhammad kuwa Mtume wangu.”[1]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Lau Muusa angelikuwa hai hii leo asingelikuwa na namna isipokuwa kunifuata.”
[1] Ahmad (3/387), ad-Daarimiy (436), Abu Ya´laa (4/102) na wengineo.
- Muhusika: Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fadhwl-ul-Islaam, uk. 18
- Imechapishwa: 23/10/2016
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)