44. Dalili kwamba Basmalah siyo sehemu katika al-Faatihah

Hakuna makinzano kati ya wanazuoni ya kwamba Basmalah ni sehemu ya Aayah ndani ya Suurah ”an-Naml”, ilihali Suurah al-Faatihah ina Aayah saba. Basi wale wanazuoni walisoema kuwa Basmalah ni Aayah kutoka ndani ya al-Faatihah wamezingatia Basmalah ndani ya zile saba. Wale walisoema kuwa siyo sehemu ya al-Faatihah wamezingatia Aayah ya saba kuwa ni:

غَيْرِ الْمَغْضُوبِ عَلَيْهِمْ وَلَا الضَّالِّينَ

“… si ya walioghadhibikiwa wala waliopotea.”[1]

Miongoni mwa dalili zinazoonyesha ya kwamba Basmalah sio Aayah ndani ya al-Faatihah ni maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) katika Hadiyth al-Qudsiy:

“Allaah (´Azza wa Jall) amesema: ”Nimeigawanya swalah baina Yangu na mja Wangu sehemu mbili na mja Wangu anapata kile anachoomba. Mja anaposema:

الْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ

”Himdi zote njema anastahiki Allaah, Mola wa walimwengu.”[2]

Allaah husema:

”Mja Wangu amenisifu…'”

Ameipokea Muslim kupitia kwa Abu Hurayrah (395). Kwa maana ya kwamba hakutaja Basmalah ndani yake.

[1] 1:6-7

[2] 01:01

  • Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbaad
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 51
  • Imechapishwa: 03/06/2026