Imaam al-Kaasaaniy amesema katika “Badaa’i´-us-Swanaa´i´”:
”Ama kuhusu kupaka juu ya soksi, ikiwa ni zenye ngozi[1] au zenye soli, basi inasihi pasi na makinzano yoyote kwa maswahiba wetu. Ikiwa si zenye ngozi wala si zenye soli, basi ikiwa ni nyembamba zinazoruhusu maji kupenya, basi haijuzu kupaka juu yake kwa maafikiano[2]. Ikiwa ni nene haijuzu, Abu Haniyfah anaona kuwa haijuzu, ilihali Abu Yuusuf na Muhammad wanaona kuwa inajuzu. Imepokelewa kutoka kwa Abu Haniyfah kwamba alirudi kwenye maneno yao mwishoni mwa umri wake. Hilo ni kwamba alipaka juu ya soksi zake katika maradhi yake kisha akawaambia waliomtembelea:
”Nimefanya lile nililokuwa nikiwazuia watu kulifanya.”
Kwa mtazamo wao wakaona kuwa hiyo ilikuwa ni dalili ya kurejea kwake… Abu Yuusuf na Muhammad wamejengea hoja kwa Hadiyth ya al-Mughiyrah bin Shu‘bah kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alitawadha na akapaka juu ya soksi. Jengine ni kwamba kujuzu kupangusa juu ya soksi za ngozi ni kwa sababu ya kuondoa uzito kwa yale yanayompata mtu katika taabu ya kuzivua, jambo ambalo ipo pia katika soksi za kawaida.”
[1] Kwa maana soksi yenye ngozi sehemu ya juu na ya chini.
[2] Kama alimaanisha maafikiano ya maimamu wa waliotangulia na wa baadaye, basi ni batili. Imam al-Nawawiy amesema katika ”al-Majmuu´”:
”Wenzetu – Shaafi´iyyah – wamenukuu kutoka kwa ´Umar na ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anhumaa) kuhusu kufaa kupaka juu ya soksi hata kama ni nyembamba. Wamenukuu pia kutoka kwa Abu Yuusuf, Muhammad, Ishaaq na Daawuud.”
Isitoshe ni maoni ya Imam Ibn Hazm, kama itakavyokuja mbele. Kwa hivyo dai la maafikiano linawezaje kuwa sahihi? Kama alimaanisha maafikiano ya Hanafiyyah, basi inaweza kukubalika. Lakini maelezo ya al-Nawawiy yaliyoko juu kuhusu Abu Yuusuf na Muhammad yanakanusha hili. Imebainika wazi kwamba hakuna maafikiano juu ya jambo hili, kwa hivyo zingatia hili!
- Muhusika: ´Allaamah Muhammad Jamaal-ud-Diyn bin Muhammad al-Qaasimiy (afk. 1332)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Mash ´alaal-Jawrabayn, uk. 66-67
- Imechapishwa: 16/04/2026
Imaam al-Kaasaaniy amesema katika “Badaa’i´-us-Swanaa´i´”:
”Ama kuhusu kupaka juu ya soksi, ikiwa ni zenye ngozi[1] au zenye soli, basi inasihi pasi na makinzano yoyote kwa maswahiba wetu. Ikiwa si zenye ngozi wala si zenye soli, basi ikiwa ni nyembamba zinazoruhusu maji kupenya, basi haijuzu kupaka juu yake kwa maafikiano[2]. Ikiwa ni nene haijuzu, Abu Haniyfah anaona kuwa haijuzu, ilihali Abu Yuusuf na Muhammad wanaona kuwa inajuzu. Imepokelewa kutoka kwa Abu Haniyfah kwamba alirudi kwenye maneno yao mwishoni mwa umri wake. Hilo ni kwamba alipaka juu ya soksi zake katika maradhi yake kisha akawaambia waliomtembelea:
”Nimefanya lile nililokuwa nikiwazuia watu kulifanya.”
Kwa mtazamo wao wakaona kuwa hiyo ilikuwa ni dalili ya kurejea kwake… Abu Yuusuf na Muhammad wamejengea hoja kwa Hadiyth ya al-Mughiyrah bin Shu‘bah kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alitawadha na akapaka juu ya soksi. Jengine ni kwamba kujuzu kupangusa juu ya soksi za ngozi ni kwa sababu ya kuondoa uzito kwa yale yanayompata mtu katika taabu ya kuzivua, jambo ambalo ipo pia katika soksi za kawaida.”
[1] Kwa maana soksi yenye ngozi sehemu ya juu na ya chini.
[2] Kama alimaanisha maafikiano ya maimamu wa waliotangulia na wa baadaye, basi ni batili. Imam al-Nawawiy amesema katika ”al-Majmuu´”:
”Wenzetu – Shaafi´iyyah – wamenukuu kutoka kwa ´Umar na ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anhumaa) kuhusu kufaa kupaka juu ya soksi hata kama ni nyembamba. Wamenukuu pia kutoka kwa Abu Yuusuf, Muhammad, Ishaaq na Daawuud.”
Isitoshe ni maoni ya Imam Ibn Hazm, kama itakavyokuja mbele. Kwa hivyo dai la maafikiano linawezaje kuwa sahihi? Kama alimaanisha maafikiano ya Hanafiyyah, basi inaweza kukubalika. Lakini maelezo ya al-Nawawiy yaliyoko juu kuhusu Abu Yuusuf na Muhammad yanakanusha hili. Imebainika wazi kwamba hakuna maafikiano juu ya jambo hili, kwa hivyo zingatia hili!
Muhusika: ´Allaamah Muhammad Jamaal-ud-Diyn bin Muhammad al-Qaasimiy (afk. 1332)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Mash ´alaal-Jawrabayn, uk. 66-67
Imechapishwa: 16/04/2026
https://firqatunnajia.com/41-madhehebu-ya-hanafiyyah-kuhusu-kupangusa-juu-ya-soksi/