al-Qummiy amesema wakati alipokuwa anafasiri Aayah:
وَلَيْسَ الْبِرُّ بِأَن تَأْتُوا الْبُيُوتَ مِن ظُهُورِهَا وَلَـٰكِنَّ الْبِرَّ مَنِ اتَّقَىٰ ۗ وَأْتُوا الْبُيُوتَ مِنْ أَبْوَابِهَا
“Na si wema kuingia nyumba kwa nyuma yake; lakini wema ni kwa kumcha Allaah. Na ingieni nyumba kupitia milango yake [ya mbele].” (02:189)
“Aayah imeteremshwa kwa mnasaba wa Kiongozi wa waumini (Rahimahu Allaah) ambaye Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema juu yake:
“Mimi ndio mji wa elimu na ´Aliy ndio mlango wake.””[1]
Hapa al-Qummiy amekusanya mambo mawili mabaya sana:
1- Amepotosha Maneno ya Allaah kutoka mahala pake na kusema kwamba Aayah imeteremshwa kwa mnasaba wa ´Aliy.
2- Ametumia dalili kwa Hadiyth iliyozushwa ambayo inanasibishwa kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kwa uongo.
[1] Tafsiyr al-Qummiy (1/68).
- Muhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 75
- Imechapishwa: 19/03/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)