383. Ni ipi hukumu ya kuzikwa Baqiy´?

Swali: Baadhi ya watu wanapofiwa na jamaa ndani au nje ya Madiynah basi wanafanya bidii azikwe sehemu ya mbele ya Baqiy´. Pengine wanaona kuwa kuna fadhilah kuzikwa sehemu ya mbele kuliko sehemu ya nyuma. Ni ipi hukumu ya hilo?

Jibu: Ikiwa maiti amekufa karibu na Madiynah basi kumzika huko ndio bora na vyema. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Ee Allaah! Wasamehe waliozikwa kwenye Baqiy´ yenye miiba.”[1]

Hata hvyo mtu asipelekwe huko kama amekufa sehemu ya mbali kutokea hapo.

Kuhusiana na kupendelea kwao kuzikwa sehemu ya mbele ya Baqiy´ kwa kudhani kuwa ndio bora, ni jambo halina msingi. Sehemu yote ya makaburi yanalingana.

[1] Muslim (974).

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/446)
  • Imechapishwa: 30/05/2026