Swali: Je, inafaa kuweka kipande cha chuma au ishara juu ya kaburi la maiti iliyoandikwa Aayah ya Qur-aan na kuongezea jina la maiti na tarehe ya kufariki kwake?
Jibu: Haijuzu kuandika juu ya kaburi la maiti si Aayah ya Qur-aan wala kitu kingine. Ni mamoja juu ya chuma, kibao wala kitu kingine. Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kupitia Hadiyth ya Jaabir (Radhiya Allaahu ´anh) kwamba:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kulitia chokaa kaburi, kukaa juu yake na kujenga juu yake.”
Ameipokea Imaam Muslim katika “as-Swahiyh” yake. at-Tirmidhiy na an-Nasaa´iy wamezidisha kwa cheni ya wapokezi Swahiyh:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kulitia chokaa kaburi, kukaa juu yake na kujenga juu yake.”[1]
[1] Muslim (970).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Tahdhiyr min Fitnat-il-Qubuur, uk. 125
- Imechapishwa: 20/07/2022
Swali: Je, inafaa kuweka kipande cha chuma au ishara juu ya kaburi la maiti iliyoandikwa Aayah ya Qur-aan na kuongezea jina la maiti na tarehe ya kufariki kwake?
Jibu: Haijuzu kuandika juu ya kaburi la maiti si Aayah ya Qur-aan wala kitu kingine. Ni mamoja juu ya chuma, kibao wala kitu kingine. Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kupitia Hadiyth ya Jaabir (Radhiya Allaahu ´anh) kwamba:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kulitia chokaa kaburi, kukaa juu yake na kujenga juu yake.”
Ameipokea Imaam Muslim katika “as-Swahiyh” yake. at-Tirmidhiy na an-Nasaa´iy wamezidisha kwa cheni ya wapokezi Swahiyh:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza kulitia chokaa kaburi, kukaa juu yake na kujenga juu yake.”[1]
[1] Muslim (970).
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Tahdhiyr min Fitnat-il-Qubuur, uk. 125
Imechapishwa: 20/07/2022
https://firqatunnajia.com/37-makatazo-ya-kuandika-chochote-juu-ya-kaburi/