Abu Muhammad ´Abdullaah bin Abiy Zayd al-Qayrawaaniy (Rahimahu Allaah) amesema:
Hana mwanzo wala mwisho.
MAELEZO
Amesema (Jalla wa ´Alaa):
هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ ۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
“Yeye ndiye wa Mwanzo na wa Mwisho na Aliye juu na Aliye karibu – Naye juu ya kila jambo ni mjuzi.” [1]
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wewe ndiye wa Kwanza; hakuna kabla yako kitu. Wewe ndiye wa Mwisho; hakuna baada yako kitu. Wewe ndiye Mwenye kudhihiri; hakuna juu Yako kitu. Wewe ndiye Mwenye kujificha; hakuna chochote chenye kufichikana Kwako.”[2]
Yeye (Subhaanahu wa Ta´ala) yuko juu ya viumbe Wake, Mwenye kudhibiti juu ya waja Wake, na hakuna kitu chenye kufichikana Kwake:
إِنَّ اللَّـهَ لَا يَخْفَىٰ عَلَيْهِ شَيْءٌ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ
“Hakika Allaah hakifichiki Kwake chochote katika ardhi wala katika mbingu.”[3]
[1] 57:3
[2] Muslim (2713).
[3] 3:5
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bayaan-ul-Ma´aaniy fiy Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy, uk. 32
- Imechapishwa: 26/07/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)