Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Imepokelewa Hadiyth Swahiyh kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Ukiwaona wale wanaofuata [Aayah] zenye kutatiza, basi [mtambue kuwa] hao ndio wale ambao Allaah amewataja [katika Qur-aan]; hivyo basi tahadhari nao!”
MAELEZO
Shaykh (Rahimahu Allaah) amesema kuwa imesihi kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Ukiwaona wale wanaofuata [Aayah] zenye kutatiza, basi [tambue kuwa] hao ndio wale ambao Allaah amewataja [katika Qur-aan]; hivyo basi tahadhari nao!”[1]
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amejengea dalili kwa Hadiyth hii ili kuthibitisha kuwa wale wenye kufuata Aayah zisizokuwa wazi maana yake katika Qur-aan, au katika Sunnah, na kuvisha batili zao hivyo viwili, hao ndio wale ambao Allaah amewataja na kuwasifu:
فَأَمَّا الَّذِينَ فِي قُلُوبِهِمْ زَيْغٌ فَيَتَّبِعُونَ مَا تَشَابَهَ مِنْهُ
“Basi wale ambao katika nyoyo zao mna upotovu hufuata zile zenye kutatiza… “
Baada ya hapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamrisha mtu kujihadhari nao ili wasikupotezeni na Njia ya Allaah kwa wao kutufanya sisi kufuata Aayah zisizokuwa wazi maana yake. Vivyo hivyo akatuamrisha kujihadhari na njia yao.
[1] al-Bukhaariy (4547) na Muslim (2665).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 57
- Imechapishwa: 11/11/2023
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Imepokelewa Hadiyth Swahiyh kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Ukiwaona wale wanaofuata [Aayah] zenye kutatiza, basi [mtambue kuwa] hao ndio wale ambao Allaah amewataja [katika Qur-aan]; hivyo basi tahadhari nao!”
MAELEZO
Shaykh (Rahimahu Allaah) amesema kuwa imesihi kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ya kwamba amesema:
“Ukiwaona wale wanaofuata [Aayah] zenye kutatiza, basi [tambue kuwa] hao ndio wale ambao Allaah amewataja [katika Qur-aan]; hivyo basi tahadhari nao!”[1]
Mtunzi (Rahimahu Allaah) amejengea dalili kwa Hadiyth hii ili kuthibitisha kuwa wale wenye kufuata Aayah zisizokuwa wazi maana yake katika Qur-aan, au katika Sunnah, na kuvisha batili zao hivyo viwili, hao ndio wale ambao Allaah amewataja na kuwasifu:
فَأَمَّا الَّذِينَ فِي قُلُوبِهِمْ زَيْغٌ فَيَتَّبِعُونَ مَا تَشَابَهَ مِنْهُ
“Basi wale ambao katika nyoyo zao mna upotovu hufuata zile zenye kutatiza… ”
Baada ya hapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamrisha mtu kujihadhari nao ili wasikupotezeni na Njia ya Allaah kwa wao kutufanya sisi kufuata Aayah zisizokuwa wazi maana yake. Vivyo hivyo akatuamrisha kujihadhari na njia yao.
[1] al-Bukhaariy (4547) na Muslim (2665).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 57
Imechapishwa: 11/11/2023
https://firqatunnajia.com/36-mlango-wa-07-matahadharisho-kwa-wale-wenye-kufuata-aayah-zisizokuwa-wazi/