Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:

Kiongozi kugawa fai na kusimamisha adhabu ni mambo yenye kuendelea. Hakuna yeyote aliye na haki ya kuwaponda wala kupambana nao.”

MAELEZO

Hapa Imaam Ahmad kabainisha haki za watawala na kwamba wao ndio wenye aki ya kugawa fai na kusimamisha adhabu. Haifai kwa yeyote kujifanyia chochote kwa mikono yake katika mambo haya. Ni katika haki zao. Kadhalika inahusiana na kumsaidia yule mwenye kukandamizwa, kutatua magomvi na mfano wa hayo.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Itmaam-ul-Minnah, uk. 139