Baada ya hapo (Rahimahu Allaah) akasema:
“Naamini kuwa Allaah ni Mwenye kufanya Akitakacho.”
Haya ni masuala mengine. Nayo ni kuhusiana na kuamini matendo ya Allaah (Jalla wa ´Alaa). Yeye ana majina, sifa, matendo na matakwa na utashi:
فَعَّالٌ لِّمَا يُرِيدُ
“Mwingi wa kufanya Atakalo.”[1]
Anaumba, anaruzuku, anahuisha, anafisha na anaendesha mambo. Haya ni matendo ya Allaah (Jalla wa ´Alaa). Yeye kwa matakwa na utashi Wake (Subhaanahu wa Ta´ala):
فَعَّالٌ لِّمَا يُرِيدُ
“Mwingi wa kufanya Atakalo.”
إِنَّ اللَّـهَ يَفْعَلُ مَا يَشَاءُ
“Hakika Allaah anafanya atakavyo.”[2]
وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَفْعَلُ مَا يُرِيدُ
“Lakini Allaah anafanya ayatakayo.”[3]
Anafanya ayatakayo na anafanya akipendacho. Maneno yake:
“Hakukuwi kitu isipokuwa kwa kutaka Kwake.”
Yanayokuwa katika ulimwengu huu ni kutokana na uumbaji Wake (Subhaanahu wa Ta´ala), matakwa na utashi Wake. Hakukuwi katika ulimwengu huu chochote pasi na matakwa Yake na uumbaji Wake na kwamba hakuna yeyote anayeumba pamoja na Allaah. Hapa kuna Radd kwa Mu´tazilah wanaosema kuwa mja anajiumbia matendo yake mwenyewe na kwamba hakuumba matendo ya waja na kwamba wao wenyewe ndio wamejiumbia nayo hali ya kujitegemea kutokamana na Allaah (´Azza wa Jall). Wanaona kuwa Allaah hana matakwa wala utashi katika matendo hayo. Sisi tunaamini kuwa matendo ya waja ni uumbaji wa Allaah na ni chumo la waja. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَاللَّـهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ
“Allaah amekuumbeni pamoja na vile mnavovifanya.”[4]
Bi maana ameumba pia yale myafanyayo.
[1] 85:16
[2] 22:18
[3] 02:253
[4] 37:96
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Aqiydat-il-Imaam Mujaddid Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab, uk. 55-56
- Imechapishwa: 18/03/2021
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)