Imaam Ahmad bin Hanbal (Rahimahu Allaah) amesema:
“Viongozi na kiongozi wa waumini wanatakiwa kusikilizwa na kutiiwa sawa wawe wema au waovu. Yule mwenye kuchukua ukhaliyfah, watu wakakusanyika juu yake na wakaridhika nao na yule mwenye kuchukua uongozi kwa mabavu mpaka akawa khaliyfah anaitwa kiongozi wa waumini.”
MAELEZO
Imaam Ahmad (Rahimahu Allaah) amebainisha kwamba ni lazima kwa kila muislamu kumtii mtawala, ni mamoja mtawala huyo ni mwema au mwovu. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Sikiliza na tii japokuwa utatawaliwa na mja wa kihabeshi aliyeadhibiwa.”[1]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“…kana kwamba kichwa chake ni kama zabibu.”[2]
Kuna Hadiyth nyingi kuhusiana na hilo ambazo mtu anatakiwa kuzirjelea.
[1] Muslim (648).
[2] al-Bukhaariy (693).
- Muhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Itmaam-ul-Minnah, uk. 137
- Imechapishwa: 29/04/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)