3- ´Aswr
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa katika zile Rak´ah mbili za mwanzo akisoma al-Faatihah na Suurah. Akirefusha kisomo katika ile Rak´ah ya kwanza zaidi kuliko anavyofanya katika Rak´ah ya pili[1]. Walikuwa wakionelea kuwa anafanya hivo ili watu waweze kuwahi Rak´ah[2].
Katika Rak´ah mbili za mwisho alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisoma kiasi cha Aayah kumi na tano, kiasi cha nusu ya yale anayoyasoma katika zile Rak´ah mbili za mwanzo katika Dhuhr. Alikuwa akifanya Rak´ah mbili za mwisho kuwa fupi kuliko zile Rak´ah mbili za mwanzo[3].
Alikuwa akisoma al-Faatihah katika zote mbili[4].
Wakati mwingine alikuwa anaweza kuwasikilizisha baadhi ya Aayah[5].
Halafu baada ya hapo anasoma Suurah tuliyoitaja katika Dhuhr.
[1] al-Bukhaariy na Muslim.
[2] Abu Daawuud kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh na Ibn Khuzaymah.
[3] Ahmad na Muslim.
[4] al-Bukhaariy na Muslim.
[5] al-Bukhaariy na Muslim.
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 100
- Imechapishwa: 06/02/2017
3- ´Aswr
Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa katika zile Rak´ah mbili za mwanzo akisoma al-Faatihah na Suurah. Akirefusha kisomo katika ile Rak´ah ya kwanza zaidi kuliko anavyofanya katika Rak´ah ya pili[1]. Walikuwa wakionelea kuwa anafanya hivo ili watu waweze kuwahi Rak´ah[2].
Katika Rak´ah mbili za mwisho alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisoma kiasi cha Aayah kumi na tano, kiasi cha nusu ya yale anayoyasoma katika zile Rak´ah mbili za mwanzo katika Dhuhr. Alikuwa akifanya Rak´ah mbili za mwisho kuwa fupi kuliko zile Rak´ah mbili za mwanzo[3].
Alikuwa akisoma al-Faatihah katika zote mbili[4].
Wakati mwingine alikuwa anaweza kuwasikilizisha baadhi ya Aayah[5].
Halafu baada ya hapo anasoma Suurah tuliyoitaja katika Dhuhr.
[1] al-Bukhaariy na Muslim.
[2] Abu Daawuud kwa mlolongo wa wapokezi Swahiyh na Ibn Khuzaymah.
[3] Ahmad na Muslim.
[4] al-Bukhaariy na Muslim.
[5] al-Bukhaariy na Muslim.
Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 100
Imechapishwa: 06/02/2017
https://firqatunnajia.com/34-kisomo-katika-aswr/