3 – Kinachofanywa juu ya nywele za kichwani kwa mwanamke ambaye kishakufa. Zinafanywa mikia mitatu na inatupwa nyuma yake. Kutokana na Hadiyth ya Umm ´Atwiyyah juu ya namna ya kumuosha msichana wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Tukazifunga nywele zake mikia mitatu na tukazitupa nyuma yake.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
4 – Hukumu ya wanawake kulisindikiza jeneza. Umm ´Atwiyyah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza:
“Tumekatazwa kufuata jeneza na wala hatukutiliwa mkazo.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Makatazo udhahiri wake ni uharamu. Maneno yake:
“… wala hatukutiliwa mkazo.”
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema juu yake katika “Majmuu´-ul-Fataawaa”:
“Makusudio yake inaweza kuwa kwamba makatazo hayakutiliwa mkazo, jambo ambalo halipingani na uharamu. Inawezekana vilevile yeye alidhani kuwa sio makatazo ya uharamu. Hoja iko katika maneno ya Mtume Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na si katika dhana ya mwengine.”[1]
[1] (24/355).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 67-69
- Imechapishwa: 06/11/2019
3 – Kinachofanywa juu ya nywele za kichwani kwa mwanamke ambaye kishakufa. Zinafanywa mikia mitatu na inatupwa nyuma yake. Kutokana na Hadiyth ya Umm ´Atwiyyah juu ya namna ya kumuosha msichana wa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Tukazifunga nywele zake mikia mitatu na tukazitupa nyuma yake.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
4 – Hukumu ya wanawake kulisindikiza jeneza. Umm ´Atwiyyah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ameeleza:
“Tumekatazwa kufuata jeneza na wala hatukutiliwa mkazo.”
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
Makatazo udhahiri wake ni uharamu. Maneno yake:
“… wala hatukutiliwa mkazo.”
Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema juu yake katika “Majmuu´-ul-Fataawaa”:
“Makusudio yake inaweza kuwa kwamba makatazo hayakutiliwa mkazo, jambo ambalo halipingani na uharamu. Inawezekana vilevile yeye alidhani kuwa sio makatazo ya uharamu. Hoja iko katika maneno ya Mtume Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na si katika dhana ya mwengine.”[1]
[1] (24/355).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 67-69
Imechapishwa: 06/11/2019
https://firqatunnajia.com/33-nywele-za-mwanamke-aliyekufa-na-mwanamke-kulisindikiza-jeneza/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)