Imaam al-Barbahaariy (Rahimahu Allaah) amesema:
17- Kuamini Muonekano siku ya Qiyaamah. Watamuona Allaah (´Azza wa Jall) kwa macho yaliyo vichwani mwao na yeye atawafanyia hesabu pasi na pazia wala mkalimani.
MAELEZO
Miongoni mwa mambo ya ´Aqiydah muhimu tena makubwa ni kuthibitisha kuonekana kwa Allaah (´Azza wa Jalla). Waumini watamuona Mola Wao siku ya Qiyaamah kwa macho yao kama wanavyouona mwezi usiku wa mwezi mng´aro na kama wanavyoliona jua waziwazi pasi na mawingu – kama ilivyokuja katika Hadiyth Swahiyh. Kumepokelewa Hadiyth nyingi zinazothibitisha waumini kumuona Mola Wao.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Sharh-is-Sunnah, uk. 72
- Imechapishwa: 27/01/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)