Tambua ya kwamba kila maandiko yenye kutaja kuwa baadhi ya matendo mema yanakifuta madhambi – kama vile wudhuu´, swawm ya Ramadhaan, swawm ya siku ya ‘Arafah na ya ´Aashuuraa’ na kadhalika – basi maana yake ni kufuta madhambi madogo, kwani hata ´ibaadah kubwa kama swalah tano, ijumaa hadi ijumaa nyingine na Ramadhaan hazifuti madhambi makubwa kwa mujibu wa Sunnah – basi vipi matendo mengine yasiyofikia daraja hizo?
Kwa hiyo wanazuoni walio wengi wanaona kuwa madhambi makubwa kama ribaa, uzinzi, uchawi n.k. hayafutwi na matendo mema peke yake – bali yanahitaji tawbah ya kweli au kutekelezwa kwa adhabu ya Kishari´ah pale panapohitajika adhabu hiyo.
Kwa hiyo ni wajibu kwa muislamu katika masiku haya yenye fadhilah afanye haraka kutubu kutokana na madhambi yote, madogo na makubwa, huenda Allaah (´Azza wa Jall) akamkubalia tawbah yake, akamsamehe madhambi yake na akakubali ´ibaadah zake. Kwani tawbah katika nyakati bora ina nafasi kubwa, kwa kuwa roho huwa zinakuwa tayari kwa ajili ya ´ibaadah na hupata tawbah ya kweli kwa sababu ya kutambua kosa, kujuta juu ya yaliyopita khaswa tukiwa kwenye mwanzo wa mwaka mpya. Hata hivyo tawbah ni wajibu katika nyakati zote.
- Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 59
- Imechapishwa: 18/05/2025
Tambua ya kwamba kila maandiko yenye kutaja kuwa baadhi ya matendo mema yanakifuta madhambi – kama vile wudhuu´, swawm ya Ramadhaan, swawm ya siku ya ‘Arafah na ya ´Aashuuraa’ na kadhalika – basi maana yake ni kufuta madhambi madogo, kwani hata ´ibaadah kubwa kama swalah tano, ijumaa hadi ijumaa nyingine na Ramadhaan hazifuti madhambi makubwa kwa mujibu wa Sunnah – basi vipi matendo mengine yasiyofikia daraja hizo?
Kwa hiyo wanazuoni walio wengi wanaona kuwa madhambi makubwa kama ribaa, uzinzi, uchawi n.k. hayafutwi na matendo mema peke yake – bali yanahitaji tawbah ya kweli au kutekelezwa kwa adhabu ya Kishari´ah pale panapohitajika adhabu hiyo.
Kwa hiyo ni wajibu kwa muislamu katika masiku haya yenye fadhilah afanye haraka kutubu kutokana na madhambi yote, madogo na makubwa, huenda Allaah (´Azza wa Jall) akamkubalia tawbah yake, akamsamehe madhambi yake na akakubali ´ibaadah zake. Kwani tawbah katika nyakati bora ina nafasi kubwa, kwa kuwa roho huwa zinakuwa tayari kwa ajili ya ´ibaadah na hupata tawbah ya kweli kwa sababu ya kutambua kosa, kujuta juu ya yaliyopita khaswa tukiwa kwenye mwanzo wa mwaka mpya. Hata hivyo tawbah ni wajibu katika nyakati zote.
Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 59
Imechapishwa: 18/05/2025
https://firqatunnajia.com/32-makusudio-ya-madhambi-yanayosamehewa/