´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia:
”Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema katika ugonjwa wake: “Mwamrishe Abu Bakr awaswalishe watu.” Nikasema: ”Abu Bakr akisimama mahali pako basi watu hawatosikia kutokana na kilio chake. Hebu mwache ´Umar aswalishwe.” Akasema: “Mwamrishe Abu Bakr awaswalishe watu.” ´Aaishah akamwambia Hafswah: “Mwambie: ”Abu Bakr akisimama mahali pako basi watu hawatosikia kutokana na kilio chake. Hebu mwache ´Umar awaswalishe watu.” Hafswah akafanya hivo ambapo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): “Hakika nyinyi ni kama wakeze Yuusuf. Mwamrishe Abu Bakr awaswalishe watu.” Hafswah akamwambia ´Aaishah: “Sikupata faida yoyote kutoka kwako.”[1]
[1] al-Bukhaariy (716) na Muslim (418).
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: as-Swalaah fiyn-Ni´aal, uk. 35-36
- Imechapishwa: 23/06/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket