31. Mabega yanatakiwa kufunikwa ndani ya swalah

Sunnah imetaja ya kuwa mwenye kuswali, pamoja na kufunika uchi wake, anatakiwa pia kufunika bega lake ndani ya swalah yake. Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Asiswali mmoja wenu ndani ya nguo moja hali ya kuwa hakuna chochote cha hiyo nguo kinachofunika mabega yake.”

Ameipokea al-Bukhaariy (359) na Muslim (1151).

  • Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbaad
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Shuruwt-is-Swalaah, uk. 33
  • Imechapishwa: 26/05/2026