Swawm ni miongoni mwa matendo bora kabisa mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala). Miongoni mwa faida za swawm ya Sunnah – mbali na thawabu zake – ni kwamba kama ilivyo kwa ´ibaadah za Sunnah nyingine, hufidia mapungufu yaliyomo katika utekelezaji wa faradhi. Miongoni mwa hayo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu swalah:
“Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amesema: ”Angalieni kama mja wangu ana swalah za Sunnah? Zitatumika kujazia mapungufu yaliyomo katika swalah za faradhi na matendo mengine yatakuwa hivyo hivyo.”[1]
Kadhalika swawm za kujitolea humsogeza mja karibu zaidi na Allaah (´Azza wa Jall) na kumpatia mapenzi Yake, kama ilivyo katika Hadiyth Qudsiy:
”Mja Wangu hatojikurubisha kwa chochote ninachokipenda zaidi kuliko yale niliyomfaradhishia. Mja wangu hatoacha kujikurubisha Kwangu kwa mambo ya kujitolea mpaka Nimpende.”[2]
[1] Ameipokea at-Tirmidhiy kwa ukamilifu wake kupitia kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) kutoka kw Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). at-Tirmidhiy amesema:
”Hadiyth ni nzuri.”
Hata hivyo ndani yake kuna Hurayth bin Qubayswah au Qubayswah bin Hurayth, ambaye ni mnyonge. Pengine at-Tirmidhiy ameifanya kuwa nzuri kwa mkusanyiko wa njia zake.
[2] al-Bukhaariy (6502).
- Muhusika: Shaykh ´Abdullaah bin Swaalih al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahaadiyth ´Ashrah Dhil-Hijjah wa Ayaam-it-Tashriyq, uk. 58
- Imechapishwa: 18/05/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket