31. Fadhilah za Mu´aadh bin ´Umar bin al-Jamuuh

126 – ´Ubaydullaah bin Sa´iyd ametukhabarisha: ´Abdur-Rahmaan ametukhabarisha: ´Abdul-´Aziyz bin Abiy Haazim ametukhabarisha, kutoka kwa Suhayl bin Abiy Swaalih, kutoka kwa baba yake, kutoka kwa Abu Hurayrah, ambaye amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Bora ya mtu ni Abu Bakr! Bora ya mtu ni ´Umar! Bora ya mtu ni Abu´Ubaydah bin al-Jarraah! Bora ya mtu ni Thaabit bin Qays! Bora ya mtu ni Mu´aadh bin ´Umar bin al-Jamuuh! Bora ya mtu ni Mu´aadh bin Jabal! Bora ya mtu ni Sahl bin Baydhwaa’!”[1]

´Abdur-Rahmaan amesema:

“Hivo ndivo alivosema; Sahl bin Baydhwaa’.”

[1] at-Tirmidhiy (3795), aliyesema Hadiyth ni nzuri, na al-Haakim (3/233 na 268), ambaye amesema Hadiyth ni Swahiyh kwa mujibu wa sharti ya Muslim. Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh Sunan at-Tirmidhiy” (3795).

  • Muhusika: Imaam Ahmad bin Shu´ayb an-Nasaa’iy (afk. 303)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwaa-il-us-Swahaabah, uk. 92
  • Imechapishwa: 15/09/2026