Swali 29: Maneno ya waliyosema kwamba kuwaraddi Ahl-ul-Bid´ah inazingatiwa ni kupambana katika njia ya Allaah ni sahihi au hayana ukweli wowote?
Jibu: Ndio. Mwenye kupambana na Ahl-ul-Bid´ah ni Mujaahid. Hili ni jambo lisilokuwa na shaka yoyote. Ahmad bin Hanbal alipoulizwa ni nani bora kati ya ambaye anafunga, anaswali, anatoa swadaqah, anafanya I´tikaaf na mambo ya kheri chungu mzima na mwengine anawaraddi wazushi, akajibu ifuatavyo:
“Ambaye anaswali, anafunga, anatoa swadaqah na anafanya I´tikaaf, haya yote ni mambo yake mwenyewe. Ama ambaye anawaraddi wazushi haya [maslahi yake yanaenea] kwa watu.”
Ni jambo lisilokuwa na shaka yoyote ya kwamba ambaye anawaraddi wazushi ni bora zaidi. Maimamu wana maneno mengi kuhusu hili.
- Muhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Fataawaa al-Jaliyyah
- Imechapishwa: 23/07/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)