93 – ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisema katika Rukuu´ na Sujuud yake:
سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي
“Kutakasika ni Kwako, ee Allaah Mola wetu, na himdi zote ni Zako. Ee Allaah! Nisamehe.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hii inafahamisha kuwa ni jambo limewekwa katika Shari´ah kusema:
سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي
“Kutakasika ni Kwako, ee Allaah Mola wetu, na himdi zote ni Zako. Ee Allaah! Nisamehe.”
katika Sujuud na Rukuu´. Lakini kusema hivo ni baada ya yeye kusema katika Rukuu´:
سُبْحانَ رَبِّيَ الْعَظِيمِ
“Ametakasika, Mola wangu, Aliye mtukufu.”
Na baada ya kusema katika Sujuud:
سُبْحَانَ رَبِّيَ الأَعْلَى
“Ametakasika, Mola wangu, Aliye juu.”
Jengine ni kwamba Rukuu´, ingawa si mahali pa kuomba du´aa, kama ilivyokuja katika Hadiyth:
“Kuhusu Rukuu´ mtukuzeni ndani yake Mola.”
Hata hivyo du´aa hii ni ndogo inayofuata baada ya Dhikr na kusifiwa kwa Allaah. Kwa hivyo tumewekewa nayo katika Shari´ah katika Rukuu´ na Sujuud.
[1] al-Bukhaariy (794) na Muslim (484).
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 96-97
- Imechapishwa: 29/10/2025
93 – ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akisema katika Rukuu´ na Sujuud yake:
سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي
“Kutakasika ni Kwako, ee Allaah Mola wetu, na himdi zote ni Zako. Ee Allaah! Nisamehe.”[1]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
MAELEZO
Hadiyth hii inafahamisha kuwa ni jambo limewekwa katika Shari´ah kusema:
سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي
“Kutakasika ni Kwako, ee Allaah Mola wetu, na himdi zote ni Zako. Ee Allaah! Nisamehe.”
katika Sujuud na Rukuu´. Lakini kusema hivo ni baada ya yeye kusema katika Rukuu´:
سُبْحانَ رَبِّيَ الْعَظِيمِ
“Ametakasika, Mola wangu, Aliye mtukufu.”
Na baada ya kusema katika Sujuud:
سُبْحَانَ رَبِّيَ الأَعْلَى
“Ametakasika, Mola wangu, Aliye juu.”
Jengine ni kwamba Rukuu´, ingawa si mahali pa kuomba du´aa, kama ilivyokuja katika Hadiyth:
“Kuhusu Rukuu´ mtukuzeni ndani yake Mola.”
Hata hivyo du´aa hii ni ndogo inayofuata baada ya Dhikr na kusifiwa kwa Allaah. Kwa hivyo tumewekewa nayo katika Shari´ah katika Rukuu´ na Sujuud.
[1] al-Bukhaariy (794) na Muslim (484).
Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ad´iyah wal-Adhkaar, uk. 96-97
Imechapishwa: 29/10/2025
https://firqatunnajia.com/28-duaa-ya-kwenye-rukuu-ii/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
