Ashaa´irah wamekuja kwa kitu ambacho ni cha ajabu kuliko maoni ya Jahmiyyah. Wamesema kwamba Qur-aan imegawanyika sehemu mbili:
Mosi: Maana.
Pili: Matamshi.
Kuhusu sehemu ambayo ni ya maana ni maneno ya Allaah. Allaah anasifika kuwa ana maneno – nayo ni ile maana iliyosimama katika nafsi. Hawaonelei kuwa Allaah anazungumza kwa herufu na sauti. Lakini hata hivyo ni maana iliyosimama juu ya nafsi Yake (Subhaanahu wa Ta´ala).
Ama matamshi wanasema kuwa yameumbwa. Wanaonelea kuwa ima ni katika maneno ya Jibriyl au ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Wameifanya Qur-aan kuwa na sehemu mbili:
Kwanza: Sehemu iliyoumbwa.
Pili: Sehemu ambayo haikuumbwa.
Kwa ajili hiyo hawakuwa pamoja na Ahl-us-Sunnah ambao wanasema kuwa Qur-aan haikuumbwa wala hawakuwa pamoja na Jahmiyyah ambao wanasema kuwa Qur-aan yote imeumbwa. Wao ni wenye kuyumbayumba. Ni kama mfano wa maneno ya manaswara juu ya al-Masiyh pale wanaposema kuwa ni binaadamu na wakati huohuo yeye ndiye Allaah. Wanaonelea kuwa al-Masiyh sehemu moja ni ya uanaadamu na nyingine ya uungu.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Sharh-is-Sunnah, uk. 68
- Imechapishwa: 22/01/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)