Swali 251: Ni matendo yepi bora anayofanyiwa maiti? Ni ipi maana ya maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Katika kuwatendea wema wazazi baada ya kufa kwao ni wewe kuwaswalia wakati wa kuswali kwako na kuwafungia wakati wa kufunga kwao.”[1]?
Jibu: Bora wanachoweza kufanyiwa maiti ni kuwaombea du´aa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Anapofariki mwanadamu basi matendo yake hukatika isipokuwa mambo matatu; swadaqah yenye kuendelea, elimu ambayo watu wananufaika nayo au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa.”[2]
Kuwaombea du´aa maiti ni bora kuliko kila kitu; ni bora kuliko kuwaswalia, kuwatolea swadaqah, kuwahijia au kuwafanyia ´Umrah. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”… au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa.”
katika mtiririko wa matendo. Ingelikuwa matendo yamewekwa katika Shari´ah kumfanyia maiti basi (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) angelisema “au mtoto mwema mwenye kumtolea swadaqah, mwenye kumfungia na kadhalika”. Wakati alipotaja du´aa basi ikatambulika kuwa kuwaombea du´aa ndio bora zaidi kuliko kumpa maiti zawadi ya matendo mema.
Kuhusu Hadiyth, neno “swalah” kunamaanishwa kuwaombea du´aa. Swalah (الصلاة) inakuja wakati mwingine ikiwa na maana ya du´aa. Allaah (Ta´ala) amesema:
خُذْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ صَدَقَةً تُطَهِّرُهُمْ وَتُزَكِّيهِم بِهَا وَصَلِّ عَلَيْهِمْ ۖ إِنَّ صَلَاتَكَ سَكَنٌ لَّهُمْ ۗ وَاللَّـهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ
”Chukua katika mali zao swadaqah uwatwaharishe na uwatakase kwazona na uwaombee duaa; hakika duaa yako ni utulivu kwao. Allaah Ndiye Mwenye Kusikia yote, Mjuzi wa yote.”[3]
[1] al-Muswannaf (3/387) kupitia kwa Ibn Abiy Shaybah.
[2] Muslim (1631).
[3] 09:103
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/276)
- Imechapishwa: 11/02/2026
Swali 251: Ni matendo yepi bora anayofanyiwa maiti? Ni ipi maana ya maneno yake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Katika kuwatendea wema wazazi baada ya kufa kwao ni wewe kuwaswalia wakati wa kuswali kwako na kuwafungia wakati wa kufunga kwao.”[1]?
Jibu: Bora wanachoweza kufanyiwa maiti ni kuwaombea du´aa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Anapofariki mwanadamu basi matendo yake hukatika isipokuwa mambo matatu; swadaqah yenye kuendelea, elimu ambayo watu wananufaika nayo au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa.”[2]
Kuwaombea du´aa maiti ni bora kuliko kila kitu; ni bora kuliko kuwaswalia, kuwatolea swadaqah, kuwahijia au kuwafanyia ´Umrah. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”… au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa.”
katika mtiririko wa matendo. Ingelikuwa matendo yamewekwa katika Shari´ah kumfanyia maiti basi (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) angelisema “au mtoto mwema mwenye kumtolea swadaqah, mwenye kumfungia na kadhalika”. Wakati alipotaja du´aa basi ikatambulika kuwa kuwaombea du´aa ndio bora zaidi kuliko kumpa maiti zawadi ya matendo mema.
Kuhusu Hadiyth, neno “swalah” kunamaanishwa kuwaombea du´aa. Swalah (الصلاة) inakuja wakati mwingine ikiwa na maana ya du´aa. Allaah (Ta´ala) amesema:
خُذْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ صَدَقَةً تُطَهِّرُهُمْ وَتُزَكِّيهِم بِهَا وَصَلِّ عَلَيْهِمْ ۖ إِنَّ صَلَاتَكَ سَكَنٌ لَّهُمْ ۗ وَاللَّـهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ
”Chukua katika mali zao swadaqah uwatwaharishe na uwatakase kwazona na uwaombee duaa; hakika duaa yako ni utulivu kwao. Allaah Ndiye Mwenye Kusikia yote, Mjuzi wa yote.”[3]
[1] al-Muswannaf (3/387) kupitia kwa Ibn Abiy Shaybah.
[2] Muslim (1631).
[3] 09:103
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/276)
Imechapishwa: 11/02/2026
https://firqatunnajia.com/251-ni-matendo-yepi-bora-anayofanyiwa-maiti/
Mshirikishe mwenzako:
- Share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Print (Opens in new window) Print
- Email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Share on X (Opens in new window) X
- Share on Pocket (Opens in new window) Pocket