Wanazuoni wamekhitilafiana kuhusu hukumu ya kuendelea kufunga bila kufuturu katika mitazamo mitatu:
1 – Kuunganisha swawm ni haramu. Haya ni maoni ya maimamu watatu; Abu Haniyfah, Maalik na ash-Shaafi’iy[1]. Ibn-ul-Mulaqqin ameegemeza maoni haya kwa kikosi kikubwa cha wanazuoni[2]. Ibn Hazm ameweka wazi juu ya uharamu wake[3]. Wamejengea hoja kwa dalili mbili:
Ya kwanza: Mantiki ya dhahiri ya katazo. Wamesema kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuunganisha swawm na Maswahabah hakukuwa ni kuwahalalishia kitendo hicho bali ilikuwa ni kuwaadhibu, kwa sababu amesema:
”… kama mwenye kuwaadhibu.”
Yale ambayo yanafanywa kwa njia ya kuadhibu hayawi ni katika Shari´ah.
Ya pili: ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Usiku ukiingia kutoka upande huu na mchana ukaondoka kutoka upande huu na jua likazama, basi mwenye kufunga ameshafuturu.”[4]
Dalili kutoka Hadiyth hii ni kuwa Shari´ah haijafanya usiku kuwa mahali pa kitu kingine isipokuwa futari na mwisho wa swawm. Hivyo kuendelea kufunga kunakwenda kinyume na mpangilio huu, kama ilivyo siku ya ‘iyd ambapo hairuhusiwi kufunga.
[1] al-Istidhkaar” (10/153) na ”al-Majmuu’” (06/318).
[2] al-I´ilaam (05/326).
[3] al-Muhallaa (07/21).
[4] al-Bukhaariy (1954) na Muslim (1100).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Minhat-ul-´Allaam fiy Sharh Buluugh-il-Maraam (05/35-36)
- Imechapishwa: 11/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)