246. Ni vipi mtu anawatendea wema wazazi baada ya kufa kwao?

Swali 246: Ni upi usahihi wa Hadiyth inayosema:

“Katika kuwatendea wema wazazi baada ya kufa kwao ni wewe kuwaswalia wakati wa kuswali kwako na kuwafungia wakati wa kufunga kwao.”[1]?

Jibu: Hadiyth hii haikusihi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Lakini katika kuwatendea wema wazazi baada ya kufa kwako ni wewe kuwaombea msamaha, kuwaombea du´aa kwa Allaah, kuwakirimu marafiki zao, kuwaunga marafiki zao na kuwaunga jamaa ambao wana mafungamano baina yako wewe na wao. Huku ni katika kuwatendea wema wazazi baada ya kufa kwao. Kuhusu kuwaswalia swalah inayotambulika kwa mujibu wa Shari´ah au kuwafungia ni jambo halina msingi wowote.

[1] al-Muswannaf (3/387) kupitia kwa Ibn Abiy Shaybah.

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/252)
  • Imechapishwa: 09/02/2026