Swali 240: Je, baba analipwa thawabu kwa pesa ambayo mtoto anamtolea kutoka katika pesa zake mwenyewe?
Jibu: Maoni sahihi ni kwamba thawabu zake zinamfikia. Imethibiti kwamba bwana mmoja alimjia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kusema:
“Mama yangu amekufa. Nafikiri kuwa endapo angeliweza kuzungumza basi angelitoa swadaqah. Je, anapata ujira ikiwa nitamtolea swadaqah?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Ndio.”[1]
Jengine ni kwamba Sa´d bin ´Ubaadah (Radhiya Allaahu ´anh) alimuuliza kama anaweza kulitoa swadaqah shamba lake kwa ajili ya mama yake ambaye kishakufa, ambapo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akampa idhini.
Hata hivyo bora ni yeye kujitolea swadaqah mwenyewe na wazazi wake awaombee du´aa. Hivyo ndivo alivyotuelekeza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pale aliposema:
“Anapofariki mwanadamu basi matendo yake hukatika isipokuwa mambo matatu; swadaqah yenye kuendelea, elimu ambayo watu wananufaika nayo au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa.”[2]
Amesema “au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa“ na hajasema amtolee swadaqah au amtendee matendo mema, ingawa mtiririko umetaja matendo.
[1] al-Bukhaariy (2670) na Muslim (1004).
[2] Muslim (1631).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/246)
- Imechapishwa: 04/02/2026
Swali 240: Je, baba analipwa thawabu kwa pesa ambayo mtoto anamtolea kutoka katika pesa zake mwenyewe?
Jibu: Maoni sahihi ni kwamba thawabu zake zinamfikia. Imethibiti kwamba bwana mmoja alimjia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kusema:
“Mama yangu amekufa. Nafikiri kuwa endapo angeliweza kuzungumza basi angelitoa swadaqah. Je, anapata ujira ikiwa nitamtolea swadaqah?” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Ndio.”[1]
Jengine ni kwamba Sa´d bin ´Ubaadah (Radhiya Allaahu ´anh) alimuuliza kama anaweza kulitoa swadaqah shamba lake kwa ajili ya mama yake ambaye kishakufa, ambapo (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akampa idhini.
Hata hivyo bora ni yeye kujitolea swadaqah mwenyewe na wazazi wake awaombee du´aa. Hivyo ndivo alivyotuelekeza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) pale aliposema:
“Anapofariki mwanadamu basi matendo yake hukatika isipokuwa mambo matatu; swadaqah yenye kuendelea, elimu ambayo watu wananufaika nayo au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa.”[2]
Amesema “au mtoto mwema mwenye kumuombea du´aa“ na hajasema amtolee swadaqah au amtendee matendo mema, ingawa mtiririko umetaja matendo.
[1] al-Bukhaariy (2670) na Muslim (1004).
[2] Muslim (1631).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (17/246)
Imechapishwa: 04/02/2026
https://firqatunnajia.com/240-je-baba-analipwa-thawabu-kwa-pesa-ambayo-mtoto-anamtolea-kutoka-katika-pesa-zake-mwenyewe/
Mshirikishe mwenzako:
- Share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Print (Opens in new window) Print
- Email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Share on X (Opens in new window) X
- Share on Pocket (Opens in new window) Pocket