24. Mjamzito na mnyonyesha wanaruhusiwa kutofunga Ramadhaan

6 – Mwanamke mjamzito na anayenyonyesha, ikiwa wataogopa madhara ya swawm juu ya nafsi zao au juu ya watoto wao, basi kila mmoja wao hula na hulipa idadi ya siku alizofungua. Ikiwa kula kwake kwake ni kwa kuogopa madhara juu ya mtoto tu, basi pamoja na kulipa swawm ataongeza kumlisha chakula masikini mmoja kwa kila siku iliyompita.

Dalili ya kufungua kwa mgonjwa mwenye maradhi sugu, mzee aliyezeeka, mjamzito na anayenyonyesha ni maneno ya Allaah (Ta´ala):

وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ

“Na ni juu ya wale wanaoiweza [kufunga swawm] lakini kwa tabu watoe fidia kulisha masikini.”[1]

Hivo ndivo alivyofasiri Ibn ´Abbaas (Radhiya Allaahu ´anhumaa). Allaah ndiye anajua zaidi.

[1] 02:184

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ithaaf Ahl-il-Iymaan bi Duruus Shahri Ramadhwaan, uk. 27-28
  • Imechapishwa: 15/02/2026