24. Hadiyth ”Nimefikiwa na khabari kuwa kuna Malaika… “

24 – Ibraahiym bin al-Hajjaaj ametuhadithia: Wuhayb ametuhadithia, kutoka kwa Ayyuub, ambaye amesema:

بلغني والله أعلم أن ملكاً موكل بكل من صلى على النبي صلى الله عليه وسلم حتى يبلغه النبي صلى الله عليه وسلم

”Nimefikiwa na khabari – na Allaah ndiye mjuzi zaidi – kuwa kuna Malaika aliyepewa kazi kwa kila anayemswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), ili iweze kumfikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”[1]

[1] Cheni ya wapokezi ya Ayyuub as-Sikhtiyaaniy ni Swahiyh. Nayo ina hukumu kinabii kwa sababu mambo kama hayo hayasemwi kutokana na maoni ya mtu. Isitoshe inatiliwa nguvu na Hadiyth ya (21).

  • Mhusika: Imaam Ismaa´iyl bin Ishaaq al-Maalikiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fadhwl-us-Swalaah ´alaan-Nabiy, uk. 38
  • Imechapishwa: 08/01/2024
  • taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy