99 – Abu Sa´iyd al-Hasan bin Muhammad bin ´Abdillaah bin Hasnuuyah al-Aswbahaaniy ametukhabarisha: Ahmad bin Ja´far bin Ma´bad as-Simsaar ametuhadithia: Abu Bakr bin an-Nu´maan ametuhadithia: Zayd bin ´Awf ametuhadithia: Ja´far bin Sulaymaan ametuhadithia, kutoka kwa Maalik bin Diynaar, ambaye amesema:
”Mwanachuoni asiyetendea kazi elimu yake ni kama vile jiwe lainI: tone linapotua juu yake, linatiririka tu.”
100 – Abul-Husayn Muhammad bin ´Abdil-Waahid bin ´Aliy al-Bazzaar ametukhabarisha: Abul-Qaasim ´Umar bin Muhammad bin Sayf al-Kaatib ametusomea: Muhammad bin al-´Abbaas al-Yaziydiy ametusomea: Abul-Fadhwl ar-Rayaashiy ametusomea:
Asiye msomi ni ambaye anasimulia elimu bila kuifanyia kazi
ambapo anajizuilia na matamanio
mpaka ayafanyie kazi yale aliyofunza –
na hapo anakuwa si mwenye kusimangwa
Ni mara chache kuna faida katika kuonelea sawa
Ikiwa matendo ya mtu si ya sawa
- Muhusika: Imaam Abu Bakr Ahmad bin ´Aliy al-Khatwiyb al-Baghdaadiy (afk. 463)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Iqtidhwaa’-ul-´Ilm al-´Amal, uk. 62-63
- Imechapishwa: 13/05/2024
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)