Tunaamini kujitokeza kwa Mnyama ardhini kutoka maeneo pake. Allaah (Subhaanah) amesema:
وَإِذَا وَقَعَ الْقَوْلُ عَلَيْهِمْ أَخْرَجْنَا لَهُمْ دَابَّةً مِّنَ الْأَرْضِ تُكَلِّمُهُمْ أَنَّ النَّاسَ كَانُوا بِآيَاتِنَا لَا يُوقِنُونَ
“Na itakapowaangukia kauli [kwa uwazi wake] Tutawatolea mnyama atembeaye katika ardhi atakayewasemezesha [aseme] kwamba watu walikuwa hawana yakini na alama Zetu.”[1]
Mnyama huyu atamuweka alama muumini na kafiri, alama itayojulisha nani ni nani. Watazungumzishwa pia; baadhi watazungumzishwa kama waislamu, wengine watazungumzishwa kama makafiri. Hiyo ndio ya maneno Yake Allaah:
تُكَلِّمُهُمْ
“… atakayewasemezesha… “
Kwa maneno yasiyokuwa ya kawaida. Hakujathibiti chochote kuhusu maeneo atakapotokea, lakini hata hivyo tunaamini kujitokeza kwake katika maeneo anayoyajua Allaah. Amesema (Subhaanah):
وَإِذَا وَقَعَ الْقَوْلُ عَلَيْهِمْ أَخْرَجْنَا لَهُمْ دَابَّةً مِّنَ الْأَرْضِ تُكَلِّمُهُمْ أَنَّ النَّاسَ كَانُوا بِآيَاتِنَا لَا يُوقِنُونَ
“Na itakapowaangukia kauli [kwa uwazi wake] Tutawatolea mnyama atembeaye katika ardhi atakayewasemezesha [aseme] kwamba watu walikuwa hawana yakini na alama Zetu.”
[1] 27:82
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 248
- Imechapishwa: 30/04/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket