´Ibaadah haisihi isipokuwa kwa masharti mawili:
Ya kwanza: Kumtakasia nia Allaah (´Azza wa Jall). Iwe imesalimika na shirki. Ikiwa iko na shirki ndani yake haikubaliwi. Amesema (Ta´ala):
وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ
”Hakika umeletewa Wahy na kwa wale walio kabla yako [kwamba]: “Ukifanya shirki, bila shaka yataporomoka matendo yako.” (az-Zumar 39:65)
وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ
“Lau wangemshirikisha bila shaka yangewaharibikia yale waliyokuwa wakitenda.” (al-An´aam 06:88)
Ya pili: Iwe imeafikiana na Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Isiwe ndani yake na Bid´ah na mambo mepya. Kutokana na maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule atakayefanya matendo yasiyoafikiana na amri yetu, basi itarudishwa mwenyewe.”
Bi maana kitendo hicho atarudishiwa mwenyewe.
Kwa hiyo yule mwenye kufanya kitu katika aina za ´ibaadah akamfanyia asiyekuwa Allaah anakuwa mshirikina. Hapajaliwi yule mwenye kufanyiwa. Ni mamoja ikawa ni sanamu, jiwe, mti, jini, mtu, ambaye yuhai au mfu. Mwenye kufanya kitu katika aina za ´ibaadah akamfanyia asiyekuwa Allaah anakuwa amemshirikisha Allaah (´Azza wa Jall).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 42
- Imechapishwa: 04/07/2018
´Ibaadah haisihi isipokuwa kwa masharti mawili:
Ya kwanza: Kumtakasia nia Allaah (´Azza wa Jall). Iwe imesalimika na shirki. Ikiwa iko na shirki ndani yake haikubaliwi. Amesema (Ta´ala):
وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ
”Hakika umeletewa Wahy na kwa wale walio kabla yako [kwamba]: “Ukifanya shirki, bila shaka yataporomoka matendo yako.” (az-Zumar 39:65)
وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ
“Lau wangemshirikisha bila shaka yangewaharibikia yale waliyokuwa wakitenda.” (al-An´aam 06:88)
Ya pili: Iwe imeafikiana na Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Isiwe ndani yake na Bid´ah na mambo mepya. Kutokana na maneno yake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Yule atakayefanya matendo yasiyoafikiana na amri yetu, basi itarudishwa mwenyewe.”
Bi maana kitendo hicho atarudishiwa mwenyewe.
Kwa hiyo yule mwenye kufanya kitu katika aina za ´ibaadah akamfanyia asiyekuwa Allaah anakuwa mshirikina. Hapajaliwi yule mwenye kufanyiwa. Ni mamoja ikawa ni sanamu, jiwe, mti, jini, mtu, ambaye yuhai au mfu. Mwenye kufanya kitu katika aina za ´ibaadah akamfanyia asiyekuwa Allaah anakuwa amemshirikisha Allaah (´Azza wa Jall).
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 42
Imechapishwa: 04/07/2018
https://firqatunnajia.com/22-ni-lazima-yapatikane-sharti-hizi-mbili-ili-ibaadah-ikubaliwe/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)