Watoto wanapofunzwa tangu wakingali wadogo basi elimu yao inakuwa yenye kubarikiwa. Elimu ni yenye kuwaathiri zaidi kuliko wanapokuwa wameshakuwa wakubwa. Kwa sababu wamekulia juu ya elimu na inakuwa imekita kwenye mioyo na ubongo wao. Ndio maana utawapata watoto ambao wameleleka juu ya kuhifadhi swalah na mafunzo juu ya ´Aqiydah na dini yao ndio vijana bora kabisa wanapokuwa wakubwa. Lakini wakiachwa na kupuuzwa, basi inakuwa vigumu kwa wazazi wao kuwalea. Mshairi amesema:
Matawi yanaporekebishwa hunyooka
lakini hayawi mepesi ikiwa yameshakuwa mbao
Malezi kwa mtoto bado akingali mdogo unaweza kumrekebisha. Lakini huwezi kumrekebisha akishakuwa mkubwa.
Baada ya hapo akamwambia mwalimu wake:
“Nikakuitikia maombi yako, kwa sababu nataraji mimi na wewe kupata thawabu za kuifunza dini ya Allaah au kulingania kwayo.”
Yule mwenye kulingania katika jambo la kheri ni kama mwenye kulifanya. Yeye na mwalimu wake wote wawili ni wenye kushirikiana katika thawabu, kwa sababu yeye ndiye ambaye kamfunza na kumwelekeza katika jambo hilo.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bayaan-ul-Ma´aaniy fiy Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy, uk. 23
- Imechapishwa: 12/07/2021
Watoto wanapofunzwa tangu wakingali wadogo basi elimu yao inakuwa yenye kubarikiwa. Elimu ni yenye kuwaathiri zaidi kuliko wanapokuwa wameshakuwa wakubwa. Kwa sababu wamekulia juu ya elimu na inakuwa imekita kwenye mioyo na ubongo wao. Ndio maana utawapata watoto ambao wameleleka juu ya kuhifadhi swalah na mafunzo juu ya ´Aqiydah na dini yao ndio vijana bora kabisa wanapokuwa wakubwa. Lakini wakiachwa na kupuuzwa, basi inakuwa vigumu kwa wazazi wao kuwalea. Mshairi amesema:
Matawi yanaporekebishwa hunyooka
lakini hayawi mepesi ikiwa yameshakuwa mbao
Malezi kwa mtoto bado akingali mdogo unaweza kumrekebisha. Lakini huwezi kumrekebisha akishakuwa mkubwa.
Baada ya hapo akamwambia mwalimu wake:
“Nikakuitikia maombi yako, kwa sababu nataraji mimi na wewe kupata thawabu za kuifunza dini ya Allaah au kulingania kwayo.”
Yule mwenye kulingania katika jambo la kheri ni kama mwenye kulifanya. Yeye na mwalimu wake wote wawili ni wenye kushirikiana katika thawabu, kwa sababu yeye ndiye ambaye kamfunza na kumwelekeza katika jambo hilo.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Bayaan-ul-Ma´aaniy fiy Sharh Muqaddimati Ibn Abiy Zayd al-Qayrawaaniy, uk. 23
Imechapishwa: 12/07/2021
https://firqatunnajia.com/21-samaki-mkunje-akingali-mbichi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)