Kuna sampuli mbili za du´aa:
1 –Du´aa kwa njia ya ´ibaadah. Ni kule kumsifu Allaah (´Azza wa Jall) katika majina, sifa na matendo Yake. Yule mwenye kusema:
سبحان الله, الله أكبر, الحمد لله
“Allaah ametakasika kutokana na mapungufu, Allaah ni mkubwa na himdi zote njema anastahiki Allaah.”
Amemuomba du´aa ya ´ibaadah.
2 – Du´aa kwa njia ya kuomba. Nako ni pale mtu anapoomba mahitaji mbalimbali kwa Allaah (´Azza wa Jall). Zote mbili zimekusanywa na Suurah al-Faatihah. Mwanzoni mwake kuna du´aa kwa njia ya ´ibaadah, mpaka katika Aayah isemayo:
إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ
”Wewe Pekee tunakuabudu na Wewe Pekee tunakuomba msaada.”[1]
Mwishoni mwa Suurah kuna du´aa kwa njia ya maombi. Wanazuoni wanasema kuwa du´aa ya ´ibaadah inapelekea katika du´aa ya kuomba, ilihali du´aa ya kuomba inakusanya du´aa ya ´ibaadah.
[1]1:5
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 220
- Imechapishwa: 16/04/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)