36 – ´Abdullaah bin Swaalih ametuhadithia: al-Layth amenihadithia: ´Uqayl amenihadithia, kutoka kwa Ibn Shihaab: Muhammad bin Jubayr bin Mutw´im amenikhabarisha, kutoka kwa Jubayr bin Mutw´im, ambaye amemukhabarisha kuwa amemsikia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akisema:

”Hatoingia Peponi mkataji.”

37 – Hafsw bin ´Umar an-Numayriy ametuhadithia: Shu´bah ametuhadithia, kutoka kwa Mujaahid bin ´Abdil-Jabbaar: Nimemsikia Muhammad bin Ka´b akisimulia kwamba amemsikia Abu Hurayrah akisimulia kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), ambaye amesema:

”Kizazi ni tawi. Kinasema: ”Ee Mola! Nimekatwa! Ee Mola! Nimedhulumiwa! Ee Mola! Ee Mola! Ee Mola!” Ndipo Akijibu: ”Je, huridhii Nimkate yule mwenye kukukata na Nimuunge yule mwenye kukuunga?”

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Ismaa´iyl al-Bukhaariy (a.f.k 256)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Birr-ul-Waalidayn, uk. 133
  • Imechapishwa: 13/01/2025