04 – Usengenyi na umbea

Miongoni mwa makosa yanayokiuka Shari´ah pia ni usengenyi na umbea. Baadhi ya wasichana – Allaah awaongoze – wanajishughulisha na kuzungumza juu ya wengine: mwanamke fulani ni mrefu, mwanamke fulani ni mfupi, mwanamke fulani ana mimba, mwanamke fulani hapendwi na mumewe, mwanamke fulani ni mnene, mwanamke fulani ni mwembamba na kadhalika. Je, hujui kuwa hayo ni haramu kwa mujibu wa Qur-aan, Sunnah na maafikiano ya ummah?

  • Muhusika: Dr. ´Abdul-´Aziyz bin Daawuud al-Faaiz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tawjiyhaat wa Tanbiyhaat lil-Fataati al-Muslimah, uk. 26
  • Imechapishwa: 15/02/2026