19. Mtume (صَلَّى اللّٰهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم) aliwapiga vita washirikina ili maombi yote afanyiwe Allaah pekee

na umehakikisha ya kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliwapiga vita ili du´aa [maombi] yote yawe kwa Allaah, nadhiri zote awekewe Allaah, kuchinja kote kuwe kwa Allaah, kuomba uokozi kote kuwe kwa Allaah na aina nyenginezo zote za ´Ibaadah afanyiwe Allaah,

MAELEZO

Bi maana baadhi asifanyiwe Allaah na baadhi akafanyiwa al-Badawiy, baadhi akafanyiwa Allaah na baadhi akafanyiwa al-Husayn. Ni lazima maombi yote afanyiwe Allaah. Ni lazima vichinjwa vyote achinjiwe Allaah. Ni lazima nadhiri na aina nyenginezo zote za ´ibaadah afanyiwe Allaah pekee. Hii ndio dini sahihi.

Ama kufanya ´ibaadah ni yenye kushirikiana baina ya Allaah na makaburi, mawalii na waja wema yote haya sio Tawhiyd. Hii ndio dini ya washirikina. Haijalishi kitu hata kama yule mwenye kufanya hivo anaitambua Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah na akawa anafunga, anaswali, anahiji, anafanya ´Umrah na mengineyo.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Kashf-ish-Shubuhaat, uk. 33
  • Imechapishwa: 03/11/2016